HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, June 20, 2016

WE ARE BACK ONLINE- Ulanga Community Resource Centre Office is at Ifakara

Dear all stakeholders

We are pleased to inform every stakeholder that our organization, Ulanga Community Resource Centre (UCRC) which is a not-for-profit organization has opened office in Ifakara.

Among other objectives, UCRC aims at:-
  1. Community empowerment on Governance and Livelihoods
  2. Promote literacy and educational activities
  3. Work on natural resource rights and management- including land rights and climate change
  4. Provision of legal aid and assistance to the poor, women, children, disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.
In order to achieve our goals we have opened our main office at Mazingira Centre, Plot no 14, Block G, Ifakara Township and we officially inform our stakeholders on our presence in Ifakara District.
As we are development stakeholder, we kindly request for strong collaboration with every development and seek your support to enhance our good objectives

 You can reach us through our address and contacts below:-

Main Office

Ulanga Community Resource Centre
P. O. Box 183,
Mazingira Centre,
Block G, Plot no 14,
Ifakara Township,
Morogoro Tanzania
Phone: +255 718-299730
Email: ucrc2012@gmail.com Internet: http://www.ucrc-ulanga.blogspot.com


Saturday, February 22, 2014

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE YA SHULE 20 ZA WILAYA YA ULANGA

JIONEE JINSI HALI ILIVYO

1.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s2469.htm Celina Kombani Secondary School
2.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s1575.htm Mtimbira Secondary School
3.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s0865.htm Igota Secondary School
4.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s4126.htm Lupiro Secondary School
5.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s0266.htm Regina Mundi  Girls Secondary
6.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s0117.htm Kasita Seminary
7.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s2474.htm Usangule Secondary School
8.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s4229.htm Sofi Secondary School
9.       http://41.188.155.122/CSEE2013/s4235.htm Igawa Secondary School
10.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s4232.htm Chilombola Secondary School
11.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s0708.htm Kipingo Secondary School
12.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s2475.htm Malinyi Secondary School
13.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s2472.htm Minepa Secondary School
14.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s2473.htm Itete Secondary School
15.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s1535.htm Nawenge Secondary School
16.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s2471.htm Uponera Secondary School
17.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s4233.htm Iragua Secondary School
18.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s4234.htm Isongo Secondary School
19.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s4231.htm Vigoi Secondary School
20.   http://41.188.155.122/CSEE2013/s4228.htm Mbuga Secondary School



Sunday, September 29, 2013

UCRC yaendesha mafunzo ya Wasaidizi wa Kisheria (Paralegal) Mtimbira

Na Francis Uhadi


UCRC ni Taasisi ya Kiraia iliyoanzishwa na kusajiliwa mwaka 2012 kama Kampuni isiyo na hisa kwa ajili ya kufanya kazi za kiraia ikiwa na usajili namba 96145 na makao yake makuu Mahenge Mjini.

Pamoja na masuala mengine, UCRC inalenga kujenga uwezo wa katika masuala ya haki za ardhi na haki rasilimali na utatuzi wa migogoro inayotokana na rasilimali hizo. Vile vile UCRC inalenga kuwawezesha wananchi wanaoishi vijijini kupata msaada wa kisheria kupitia usaidizi wa kisheria.  UCRC inaamini kuwa Wananchi wakiwezeshwa kupata taarifa sahihi juu ya masuala mbalimbali wataweza kusimamia kikamilifu shughuli mbalimbali za jamii ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha viongozi wao  na hivyo kuleta maendeleo.

UCRC ikiwa ni Taasisi changa na ikiwa bado katika kipindi cha kutafuta fedha kwa ajili ya kujiendesha, imeandaa mafunzo ya siku 6 kwa Wasaidizi wa Kisheria (Paralegals). Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo vijana ili waweze kutumika katika jamii kama wasaidizi wa kisheria katika masuala mbalimbali yanayoikabili jamii.


SAFU YA UONGOZI WA KITUO CHA USAIDIZI WA KISHERIA MTIMBIRA


M/kiti wa Paralegal Ndg. Cloud Masekesa
Katibu wa Paralegal Bi Maria Mhaville
Mweka Hazina wa Paralegal Bi Jackline Luselo


Awali matangazo yalitolewa makanisani, misikitini, na maeneo mbalimbali kuwataka vijana waliomaliza kidato cha nne na wenye uwezo wa kujieleza na kuchambua masuala mbalimbali wajitokeze. Zoezi la kuwapata vijana hao lilichukua takriban mwezi na siku kadhaa. Vijana zaidi ya 40 walijitokeza hata hivyo wengi walifikiri hii ni kazi ya kulipwa mshahara. Waliposikia kuwa hakina mshahara wengi waliondoka na wengine walichujwa kutokana na kushindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa.

Mhe. Diwani wa Kata ya Mtimbira Ndg. Richard Likalangu akifungua mafunzo ya Wasidizi wa Kisheria yaliyoanza siku ya Jumatatu Tarehe 23 Septemba 2013. Mafunzo hayo yanatarajia kumalizika tarehe 2 Octoba 2013

Kwa kuwa Taasisi haijapata fedha kutoka kwa mfadhili yeyote, shughuli hii imegharimiwa na waanzilishi wa Taasisi hiyo. Jumla ya vijana 8 ambapo Wasichana ni 3 na Wavulana 5 wamepata mafunzo hayo.

Mafunzo hayo yatchukua muda wa majuma mawili ambapo awali vijana hao walifundishwa dhana nzima ya Usaidizi wa Kisheria na Miiko yake, jinsi ya kuenenda kama msaidizi wa kisheria na maadili katika usaidizi wa Kisheria.

Vijana hao pia walifundishwa Sera na Sheria mbalimbali zikiwemo Sheria za Ardhi za mwaka 1999 na mfumo wa utatuzi wa Migogoro ya Ardhi. Pia katika juma la kwanza wamefundishwa juu ya Haki za Binadamu pamoja na sharia ya makosa ya Jinai.

Katika juma la pili ambalo linaanza kesho tarehe 30 Septemba vijana hao watafundishwa sheria za Miradhi, Watoto na Haki za Wanawake na Watoto

Ni matarajio yetu kuwa mafunzo haya watatoa vijana ambao watatumika katika kutoa ushauri wa Kisheria kwa wanachi  ili kusaidia kutatua migogoro mbalimbali na hivyo kuleta ufanisi kwa kuwafanya wananchi kupata haki zao. 

Katika picha ni Mhe. Diwani wa Kata ya Mtimbira na Vijana wanoandaliwa kupata mafunzo ya Usaidizi wa Kisheria mara baada ya kufungua rasmi mafunzo hyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kata ya Mtimbira

Baadhi ya Waidizi wa Kisheria mara baada ya kumaliza mafunzo katika wiki ya kwanza.

Shukrani zetu za dhati kabisa ziwafikie viongozi mbalimbali wa Serikali kwanza pale Mtimbira ambapo kabla ya mafunzo haya mwandaaji alijitahidi kuonana na Mheshimiwa Diwani Ndg Richard Likalangu, Asisa Mtendaji Kata Ndugu Rajab Mgululi, Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mtimbira Bi Rehema Salumu na Mkuu wa Kituo kidogo cha Polisi Mtimbira kwa lengo la kutambulisha kwao dhana ya Usaidizi wa Kisheria. Pamoja nao Katibu wa Baraza za Kata pia alishiriki katika mafunzo.

Mwitikio ambao umepatikana kwa viongozi hao ni wa kuigwa katika maeneo mengine kwani wote kwa ujumla wao walifurahishwa sana na kuanzishwa kwa Taasisi hii lakini pia kuleta mafunzo ya usaidizi wa kisheria. Kwa upande wake Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mtimbira alisema kuwa ni matarajio yake kuwa kuanzishwa kwa kituo cha Usaidizi wa Kisheria Mtimbira kutapunguza mlundikano wa kesi zisizo za lazima kufikishwa Mahakamani. Hivyo aliwataka vijana waliofundishwa kuchapa kazi kwa weledi na wananchi kukitumia kituo hiki ili kiwe msaada kwao.

Kwa namna ya pekee, kama sehemu ya Mchango wao wa awali, Afisa Mtendaji Kata ya Mtimbira Ndg. Rajab Mgululi alitoa bure ukumbi wa Kata ili kufanyia mafunzo. Pia kwa kushirikiana na Mhe. Diwani pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mtimbira wameahidi kutoa jengo moja litumike kama ofisi ya awali ya Wasaidizi wa Kisheria. Hii ni hatua kubwa sana katika kufanikisha kazi hii ya usaidizi wa Kisheria katika Ulanga.

Ni malengo ya Taasisi kuanzisha vituo vya usaidizi wa kisheria maeneo mengi zaidi ikiwa na uwezo.

Tunakaribisha maoni, ushauri na michango mbalimbali ya hali na mali ili Taasisi hii iweze kusimama. Kama utapenda kuchangia au kutoa mawazo yako au maoni yako usisite kutuandikia: ucrc2012@gmail.com au kutupigia simu +255 755831152

UCRC- Lean.Analyse.Take Action


Friday, March 8, 2013

IFAKARA WAADHIMISHA SIKU YA MMWANAMKE DUNIANI

MAADHIMISHO SIKU YA MANAWAKE DUNIANI IFAKARAYAFANA


MWANACHAMA WA KIKUNDI CHA KIWAKIKI AKIBEBA BANGO KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MJINI IFAKARA 
WANAWAKE WAKIWA KATIKA MAANDAMANO KUELEKEA KIUNGANI KWA MAADHIMISHO
WANAWAKE WAKIWA NA NYUSO ZA FURAHA KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

MAANDAMANO YANAENDELEA
WAKINA DADA NAO WAKIWA KATIKA MAANDAMANO

Wednesday, February 20, 2013

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 BAADHI YA SHULE KATIKA WILAYA YA ULANGA

Ndugu wapendwa, tunafahamu kuwa kwa matokeo ya Form 4 ya mwaka 2012 kuwa takriban asilimia 60 ya watahiniwa wamepata SIFURI. Katika hali hiyo kwa mazingira ya Ulanga ni mbaya zaidi. Tumejaribu kuweka links za baadhi ya shule hapo chini jioneeni wenyewe. 


BAADHI YA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MTIMBIRA 

Pamoja na ubaya wa matokeo hayo, tunawapongeza baadhi ya vijana walioweza kupata angalau daraja la tatu pamoja na wale waliopata la nne wenye points zinazowawezesha hata kwenda ualimu. Kwa wengine ndo hivyo mambo yamekuwa magumu. Lakini tunapenda pia kuwa wakweli hapa, pamoja na miundo mbinu isiyoridhisha ya shule na kadahlika, wapo baadhi ya wanafunzi wa shule hizi hawakupenda kutumia nafasi yao vizuri ikiwa ni pamoja na walimu waliopo katika shule hizo. Mfano, wapo walimu au vijana ambao wapo vyuoni huwa wanajitolea kufundisha ama bure au kwa kuchangia kidogo sana, lakini mwitikio wa wanafunzi umekuwa duni sana. Mara nyigngi tumetembelea baadhi ya shule kama vile pale Mtimbira na kuongea na wanafunzi, bado mwamko wa kutumia muda wao kuhusu masuala ya shule ni mdogo sana. Itakumbukwa kuwa miaka ya 80 na 90 na miaka ya awali ya 2000 mambo ya masomo ya ziada ilikuwa ni ngumu sana kuyapata lakini sasa wapo vijana wengi waliohitimu elimu ya juu wanatoka maeneo tunayozungumza. Tunawaomba tufanye kazi ya ziada kuokoa jahazi hili linalozama. 

suala lingine linaloharibu maendeleo ya wanafunzi katika wilaya za ulanga na kilombero ni NGONO. Tunaomba tu tuwe wawazi hapa. Kuna hawa jamaa wanao nunua Mpunga na sasa vijana wa Boda Boda wanawamaliza wasichana katika Wilaya hizi. Lakini poa kuna watu wa mitaani na miongoni mwa wanafunzi wenyewe suala la ngono limekuwa likiendelea kwa kasi sana. Katika  hali kama hiyo kufeli kutaendelea. 

Mwisho kumeingia suala la USHAROBARO hasa wilaya ya Ulanga. Ni kituko, vijana wengi wa kiume wanatumia mda mwingi katika UNNECESSARY businesses kuliko kusoma. Hatutaweza kubadili hali hii ya kushindwa katika mitihani kama hatutakuwa na mabadiliko toka ndani. 

USHAURI WANGU

Kuna mambo mengi tunaweza kufanya lakini naomba ni yaache yote na nilizungumzie moja la wanafunzi wa elimu ya juu kufundisha katika shule mbalimbali Ulanga na Kilombero. Natoa mapendekezo kuwa tuandae orodha ya wanafunzi wote wanaotoka katika wilaya za Ulanga na Kilombero waliopo katika vyuo vikuu na colleges ikiwa ni pamoja na taaluma zao. Sisi tulio makazini tuanzishe MFUKO WA ELIMU ambao utawawezesha hao wanafunzi kwenda kufundisha wakati wa likizo na tukawapatia angalau nauli. Pia kwa wale wanaosoma ualimu wahamasishwe kuomba FIELD ATTACHMENT katika shule za Ulanga na Kilombero ili kuinua kiwango cha elimu katika Wilaya hizo.

Hayo ni mawazo yangu, wewe una mawazo gani???? funguka sasa

Jionee matokeo ya Baadhi ya Shule




SOFI SECONDARY http://www.jamiiforums.com/matokeo2012/data/s4229.htm


http://www.necta.go.tz/matokeo2012/csee2012/data/s2469.htm



CLICK TO SEE THE RESULTS





Thursday, January 31, 2013

JESHI LA POLISI YASUSIWA MAITI YA MFUGAJI MOROGORO.


MAUAJI YA MFUGAJI ULANGA MOROGORO

Habari yote kwa Hisani ya Juma Mtanda, Morogoro




 Mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti kushoto akizungumza na wafugaji (hawapo pichani) baada ya wafugaji hao kususia maiti kwa siku mbili wakidai mpaka serikali itimize masharti yaliyowekwa na familiakushoto ni Kamanda wa polisi Morogoro Shilogile na katikati ni Mwenyekiti wa ccm wilaya ya Ulanga Halidi Nalyoto.
 Mkuu wa wilaya ya Ulanga, Francis Miti kulia akimsikiliza Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile kushoto baada ya kamanda huyo kukataliwa na familia ya marehemu Baya Kidinga (20) kutambua mwili wa marehemu kisha kukubali kuupokea na kwenda kuuzika.



Sehemu kubwa ya wafugaji wilaya ya Ulanga wakimsubiri mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti baada ya familia ya marehemu kukataa kutambua mwili wa marehemu ndugu yao anayedaiwa kupigwa risasi na askari polisi waliokuwa katika zoezi la udhibiti na ufuatilia wa mifugo katika hifadhi ya bonde la mto Kilombero kuupokea na kwenda kuulizika yaliyotolewa na kamanda wa polisi ya mkoa Morogoro huo. 



 Mmoja wa wafugaji akizungumza jambo mbele ya Kamanda wa polisi hayupo pichani. 


 Kitambulisho cha marehemu Baya Kidinga (20) cha kuhitimu mafunzo yaMgambo mkoa wa Morogoro.



 Marehemu Baya Kidinga (20) enzi za uhai wake.


 Eneo ambalo linadaiwa marehemu Baya Kidinga (20) alipigwa risasi na kufariki dunia baada ya askari polisi kumfyatulia na kupoteza maisha damu ikiwa imetapakaa chini, picha iliyopigwa januari 27/ 2013.

 Sehemu ya wafugaji wa jamii ya wasukuma wakimsikiliza kamanda wa polisi Morogoro (hayupo pichani) wakati wa tukio hilo. 


Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jidai mkoa wa Morogoro Hamis Seleman kulia akimsihi ndugu wa marehemu,Baya Kidinga (20), Madaha Shirinde baada ya kususia maiti mpaka serikali itimize mashrti yaliyowekwa na familia hiyondipo wakulibali kuchukua mwili na kuuzika.



Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile kushoto akimsikiliza Manogeleku Kisandu kulia ambaye ni shahidi aliyeshuhudia tukio la kupigwa risasi marehemu Baya Kidinga (20) na askari polisi januari 31/ 2013 katikaKitongoji cha Lugangeni Kijiji cha Ipera Asilia Tarafa ya Mtimbira wilaya ya Ulanga Mkoani hapa.




 Baba mzazi wa marehemu, Baya Kidinga (20), Katambi Jidiga (katikati) akibembelezwaa na mtoto wake Madaha Shirime kushoto na afisa mtendaji kijiji cha Ipera Asilia, Zikeni Magoha kulia.

JESHI LA POLISI YASUSIWA MAITI YA MFUGAJI MOROGORO


 Baba mzazi wa marehemu, Baya Kidinga (20), Katambi Jidiga kulia akimsikiliza Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile kulia akimweleza jambo juu ya tukio la mauaji ya mtoto wake lililotokea januari 26/ 2013 baada ya kudaiwa askari polisi waliokuwa katika zoezi la udhibiti na ufuatilia kumpiga risasi.

HABARI KAMILI HII HAPA.


JESHI la polisi Wilayani Ulanga Mkoani Morogoro limelazimika kurudisha jumla ya sh 10 milioni zinazodaiwa kuporwa kwa mfugaji wa jamii ya kisukuma baada ya kumuuwa kwa kupigwa risasi mdogoni hatua hiyo ilikuja baada ya kususiwa maiti hiyo kwa siku mbili.

Hatua ya utekelezaji wa urudishaji wa pesa hizo zilizokuwa zikilalamikiwa na ndugu wa mfugaji huyo aliyefahamika kwa jina la Baya Katambi Kidiga ni sehemu ya makubaliano yaliofikiwa mbelee ya Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Francis Mitti na Mkuu wa jeshi la polisi Mkoani hapa Faustine Shilogile, Mkuu wa upelelezi makosa ya jinai mkoani hapa Hamisi Selemani, Mkuu wa polisi Ulanga.

Sakata hilo la mauaji na uporaji linaloendelea kulichafua jeshi la polisi Mkoani Morogoro limetokea tarehe 26, January 2013 katika Kitongoji cha Lugangeni Kijiji cha Ipera Asilia Tarafa ya Mtimbira wilaya ya Ulanga Mkoani hapa.

Awali polisi hao walidaiwa kutekeleza mauaji hayo majira ya saa 4 kwa kumpiga risasi marahemu huyo na kuuchukua mwili wake na kuupeleka kituo cha afya Mtimbira haraka haraka kwa kutumia gari la polisi linalodaiwa likishiriki katika operationi ya kukamata mifugi wilayani humo kutoka kwenye hifadhi ya bonde la mto Kilombero.

Baadhi ya masharti ambayo polisi walitakiwa kutekeleza ni kutoa ripoti ya kina ya uchunguzi wa kifo kutoka kwa daktari ambao utabainisha kuwa marehemu Baya Kidinga (20) amefariki dunia kwa kupigwa kwa risasi.

Hatua ambayo jeshi hilo lilitekeleza kwa kutoa ripoti daktari alitoa riporti ya mauaji hayo yaliodhibitisha bila shaka kuwa ameuwawa kwa kupigwa risasi ambayo ilikubaliwa.

Sharti la pili ambalo polisi walitakiwa kutekeleza ni kujua ni kwanini mwili wa marehemu ulihamishwa toka katika eneo la tukio kwa haraka bila hata kutoa fursa ya ndugu zake kuwepo na baadhi ya ndugu na majirani waliokuwa waliotaka kufuatilia juu ya mkasa huo walizuiwa.

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alikuwa wa kwanza kuonja makali ya wananchi ambapo aliwasili majira saa saa 5 asubuhi siku ya tukio na jopo la maafisa wa jeshi hili huku idadi ya wafugaji wakiendelea kukusanyika kwa kuulizwa maswali yaliomshinda ikiwemo kutakiwa kueleza kama operationi ya kuwaondoa wafugaji katika hifadhi ya bonde la mto Kilombero ipo au imekwisha na eneo ambalo marehemu ameuwawa ndani ya hifadhi ama laa.

Shilogile akijibu maswali hayo alisema kuwa operationi anachojua yeye ilisitishwa katika wilaya ya Kilombero lakini kwa wilaya ya Ulanga hilo hatakuwa na jibu la swali hilo lakini swahili litajibiwa na mkuu wa wilaya ya Ulanga pindi atapofika.

“Poleni kwa msiba huu mimi nimekuja na timu ya wenzangu akiwemo mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai mkoa wetu lakini natumaini kila kitu kitaenda sawa na kingine mimi nimekuja eneo la tukio kutaka kujua ukweli wa tukio hili ili kubaini ukweli wenyewe ikiwemo nani amefanya kosa na mpaka sasa askari wetu waliohusika katika tukio hilo tayari tunawashikilia kwa ajili ya uchunguzi wa awali na wakibaini sheria itachukua mkondo wake” alisema Shilogile.

Kamanda huyo ambaye alikabiliwa na maswali mengi kutoka kwa wafugaji hao likimwemo la msemaji wa familia hiyo ya marehemu, Baya Kidinga (20), (Madaha Shirinde) aliyeuliza kwa kutaka ufafanuzi wa kina kwa kuuliza swali je askari aliyepata mafunzo anapaswa kufanya nini pindi anapokabiliana na mtu mwenye silaha za asili ikiwemo fimbo ? ama kutuliza ghasia au vurugu anapaswa kutumia bunduki kwa kupiga mwananchi katika eneo gani ?.

Akijibu maswali hayo Kamanda wa polisi Morogoro, Shilogile alijibu kuwa anapaswa kumpiga mtu risasi kwa kutumia bunduki kwenye miguu na kueleza kuwa yeye amefika eneo hilo na timu yake kwa lengo la kujua mazingira ya tukio lililivyofanywa na askari baada ya kufanya uchunguzi na kuwahoji walioshuhudia.

Majibu hayo ya kamanda yalizusha mzogo mkali kutoka kwa wananchi hao na kuzalisha maswali mengine likimo la kuhoji kwanini askari wako ametumia silaha kwa kumpiga marehemu risasi mdogoni kama amepata mafunzo ?.

Kamanda huyo alieleza tena kwa umati wa wafugaji hao kwa kusema kuwa kwa wakati huo atakuwa na jibu la swali hilo na kuongeza hawezi kujua kilichompata askari huyo mpaka ametumia silaha kwa kumpiga risasi marehemu jambo hilo tutalifanyia kazi baada ya kukabilika kwa uchunguzi wao. 

Maswali hayo hayakuweza kuwaridhisha umati wa wananchi na upande wa familia ya marehemu na kumtaka kamanda huyo awasiliane na mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti kwa kuhoji kwa nini wewe Kamanda umetembea umabli mrefu kufika eneo la tukio na mkuu wako wa wilaya ambaye yupo jirani ameshindwa kufika eneo la tukio ?.

Mzozo huo ulidumu kwa muda wa masaa mawili bila kufikia muafaka katika siku ya pili baada ya tukio kutokea ambayo kamanda wa polisi alishindwa kutimiza malengo yake, likiwemo kuwashawishi ndugu wa marehemu wakubali kuutambua mwili wa marehemu, kupokea uchunguzi wa daktari na kuchukua mwili wa marehemu jambo ambalo alilazimika kuwasiliana na mkuu wa wilaya ili kufika eneo la tukio.

DC ULANGA.
Mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti aliwasili katika eneo la tukio la mjira ya saa 10:30 alasiri na kuanza kuwapa pole umati uliokuwa ukimsubiri ili kutatua kero za wananchi hao.

Miti baada ya kutoa pole kwa wafiwa alianza kutoa ufafanuzi juu ya zana iliyojengeka kwa wananchi hao kuwa marehemu amepigwa risasi katika zoezi la operesheni na kuwa askari hao hawakuwa katika operesheni bali walikuwa katika zoezi la udhibiti na ufuatiliaji wa mifugo katika bonde la hifadhi mto wa Kilombero na kuwa wanaobainika hukamatwa na kutozwa faini kisha kuwapa ovyo waliende tena katika bonde la mto Kilombero.

“tukio hili hakuna anayefurahia hata kidogo niwaeleze kuwa operesheni haipo kilichopo sasa ni udhibiti na ufuatiliaji wa mifugo katika bonde la hifadhi mto wa Kilombero na operesheni tayari ilishaisha tangu januari mosi mwaka huu” alisema Miti.

Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya naye alikumbana na maswali juu ya watendaji wake waliokuwa katika operesheni na udhibiti na ufuatiliaji wa mifugo katika bonde la hifadhi mto Kilombero na kuwa daktari wa mifugo wilaya Ulanga, Fredrick Sagamiko amekuwa akidaiwa kukiuka utaratibu wa faini.

Mselengeti Mipawa (41) alimweleza mkuu wa wilaya katika tukio hilo kuwa daktari huyo amekuwa akitoza faini kati ya sh60,000 hadi 100,000 pindi anapokamata mifugo badala ya faini iliyoidhinishwa na serikali ya kiasi cha sh44,000 kwa ng’ombe mmoja jambo ambali wamekuwa wakilipia na kuwarudisha nyumba katika harakati za maendeleo.

Mipawa alimweleza mkuu huyo wa wilaya kuwa daktari huyo wa mifugo wilaya ya Ulanga, licha ya kukiuka utozaji wa faini pia amekuwa akimakata na mifugo ambayo haiku kwenye listi ya ukamataji wa operesheni hiyo wakiwemo kukamata mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na punda na kutozwa faini kubwa kuanzia kiasi cha sh 700,000 na kuendelea kulinagana na uwingi wa mifugo hiyo.

Miti alisema kuwa baada ya kupata tuhuma zinazo mwelekeza daktari wa mifugo wilaya Ulanga, Fredrick Sagamiko yeye atawasilisha tuhuma hizo kwa mwajili wake ambaye ni mkurugezi wa halmashauri ya wilaya ya Ulanga ili uchunguzi ufanyike na kama itabainika sheria itafuata mkondo wake.

Aliwaeleza umati huyo kwa kuwataka wafugaji waache tabia ya kuwashambulia askari na kuwataka askari nayo kutotumia nguvu kubwa wakati wa vurugu pindi inapotokea hiyo itasaidia kuendeleza ushirikiano mzuri baina ya jeshi la polisi na wananchi.

Mkuu huyo alilazimika kuwashawishi ndugu wa marehemu wakubaliane na ombi lao la kutaka wakatambue mwili wa marehemu na kupokea uchunguzi wa daktari kisha kuchukua mwili wa marehemu kwa ajili ya mazishi jambo ambalo lilishindikana kukubali ombi hilo kutokana na kutotimiza madai yao.

Baada ya Kamanda wa polisi na mkuu wa wilaya Ulanga kushindwa kuwashawishi ndugu wa marehemu kuchukua mwili wa ndugu yao msafara wao uliondoka eneo hilo majira ya saa 12:30 jioni na siku ya pili ya januari 28 mwaka huu ikifuatiwa na kutokubaliana hadi gazeti hili liondoka katika eneo la tukio.

Awali Baba wa marehemu Katambi Jidiga alisema kuwa marehemu alitokea mkoani Songea kuuza baadhi ya ng’ombe kwa ajili kulipa madeni ya mifugo iliyokamatwa katika operationi, awali imetajwa mbuzi 100 alilipa lakini saba, ngombe inadaiwa akikuwa akidaiwa 10 milioni na mara ya tatu ngombe wake waliokamatwa na askari hao alikuwa akidaiwa sh milioni 3.