HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, October 11, 2012

SHAMBA DARASA KUPUNGUZA TATIZO LA MAAFISA UGANI


Na Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero

MBINU ya Shamba Darasa inatarajiwa kusaidia kupunguza tatizo la Uhaba wa Maafisa Ugani Vijijini.

Juliana Njombo,Mwezeshaji wa Shamba Darasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero amewaambia Washiriki wa Mafunzo kwa Wataalamu wa Kilimo kuhusu Dhana ya Shamba Darasa kuwa Mkulima aliyeshiriki ipasavyo katika mafunzo ya Shamba Darasa anakuwa Mtaalamu na anauwezo wa kusaidia Wakulima Wengine.

Amesema Kuwa pindi mkulima anapowezeshwa na mwezeshaji wa Mafunzo ya Shamba Darasa anakuwa Mtaalamu baada ya Kuhitimu naye anawafundisha wenzake na kutanua wigo kwa wakulima wengine katika kila kipindi cha msimu wa Kilimo na hivyo kusaidia kupunguza tatizo la Maafisa Ugani katika baadhi ya Vijiji.

Lengo kuu la Mafunzo hayo ya Siku Nne yanayoshirikisha Maafisa Ugani wa Vijiji Saba,Wataalamu kutoka Ofisi ya Kilimo Wilaya ya Kilombero Wawili,wawezeshaji Wawili na watu wa Kada nyingine Jumla yao 15 ni washiriki kuweza kupata ujuzi wa kuanzisha na kuendesha shamba Darasa katika Maeneo husika.

Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Wawezeshaji kutoka Idara ya Kilimo ya Halmashauri ya Kilombero inasimamiwa na Shirika lisilo la Kiserikali linalojihushisha na Mazingira katika Bonde la Kilombero (KIVEDO) chini ya Ufadhili Serikali ya Ujerumani kupitia Wizara ya Uchumi na Maendeleo kupitia Plan International.

 

No comments:

Post a Comment