HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, January 17, 2013

IFAKARA yamlilia Regia Mtema


Senior Libonge,Ifakara


WAKAZI wa mji wa Ifakara wilayani Kilombero jana wamefanya maandamano ya amani ya kumkumbuka ya mwaka mmoja tokea kitokee kifo cha aliyekuwa mbunge wa viti maalum katika jimbo la Kilombero Regia Mtema ambapo maandamano hayo yalipokelewa na mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala.

Maandamano hayo yalianzia katika kituo cha mafuta cha Ester kisha kumalizikia katika makaburi ya Lipangalala ambapo marehemu ndipo alipozikwa na baada ya kufika hapo shughuli za kuweka mashada ya maua na kuwasha mishumaa zilifanyika na zote hizo ziliongozwa na Masala na famila ya marehemu kupitia Regia Mtema Foundation.





MKUU wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala akiwasha ishara katika kaburi la aliyekuwa mbunge wa viti maalum jimbo la Kilombero Regia Mtema ikiwa ni ishara ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kwa kifo chake

Licha ya kufanya maandamano hao ya amani Regia Mtema Foundation siku moja kabla ya maandamano hayo kwa kushirikiana na wananchi mbalimbali walipanda miti katika shule mbalimbali za msingi zilizopo katika mji wa Ifakara na zoezi la mwisho kufanyika ni kutoa misaada mbalimbali katika kituo cha kulelea watoto wenye matatizo ya akili cha Bethlehem kilichopo Kibaoni mjini Ifakara.

Shughuli za kumkumbuka marehemu Regia Mtema zilifanyika pia jijini Dar es Salaam hapo Januari 14 katika hoteli ya Peacock ambapo  mada mbalimbali ziliwasilishwa na kujadiliwa kama alivyozisimamia marehemu ikiwemo historia ya Regia iliyowasilishwa na Mbunge David Kafulila,mada juu ya rushwa iliyowasilishwa na Takukuru na Ulemavu sio kutoweza iliyowasilishwa na Shida Salum mwenyekiti wa CHAWATA

MKUU wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa mbunge wa viti maalum jimbo la Kilombero Regia Mtema baada ya kupokea matembezi ya mshikamano yaliyofanywa na wananchi wa Kilombero katika kumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kifo chake

Pia Mh January Makamba aliwasilisha mada ya nafasi ya kijana katika kuchochea maendeleo na demokrasia,makala za Regia na pia nasaha kutoka kwa wabunge  Mh Zito Kabwe na John Mnyika,Hussen Bashe na mzee Mtema zilitolewa.

WAKAZI wa mji wa Ifakara wakiwa katika matembezi ya mshikamano ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kitokee kifo cha mbunge wa viti maalum jimbo la Kilombero Regia Mtema.(Picha zote na Igamba Libonge).


Marehemu Regia Mtema alifariki kwa ajali ya gari katika eneo la Ruvu Januari 14 mwaka jana baada ya gari alilokuwa akiliendesha kupinduka na kusababisha kifo chake na baadaye kuzikwa mjini Ifakara katika mazishi yaliyokusanya watu wengi na kuongozwa na Rais Jakaya Kikwete

No comments:

Post a Comment