Na
Senior Libonge,Kilombero
WITO umetolewa kwa askari wa kambi
ya Jeshi la Kujenga Taifa(JKT Chita) kujiwekea malengo yao hasa katika suala la
elimu ili kuweza kutimiza ndoto zao pamoja na za familia zao.
Akizungumza
na askari hao katika tafrija ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka mpya
sambamba na kumpongeza mkuu wa kikosi hicho Meja Msabaha Yamawe kwa kupata
shahada ya pili ya uzamili ya uhasibu na fedha,mkuu wa wilaya ya Kilombero
Hassan Masala amesema kuwa moja ya majukumu ya kutimiza malengo yako ni kupata
elimu.
Masala
amesema kinachofanyika hivi sasa kwa askari nchini ni kubweteka baada ya kupata
ajira bila kufahamu kuwa kujiendeleza kwa elimu ni kupiga hatua moja zaidi ya
maisha hasa katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia.
Amempongeza
mkuu wa kikosi hicho kwa kujiendeleza na kupata shahada ya pili bila kuridhika
na mamlaka makubwa ya kuwaongoza wenzie na kusema kuwa kiongozi huyo amekuwa
mfano mzuri kwa wenzie hivyo na askari waliopo chini yake pia waige mfano huo.
Masala
amemtaka mkuu huyo wa kikosi kunufaisha wenzake kwa elimu aliyoipata na kuwa
mfano bora kwa wafanyakazi wenzie na familia yake na hasa kuwaruhusu wale wote
wanaotaka kujiendeleza ili mradi wafuate sheria za kijeshi.
Naye
meja Yamawe amemuhakikishia mkuu huyo wa wilaya kuwa elimu aliyoipata ataitumia
kwa faida ya jeshi na taifa kiujumla na kusema kuwa alikwisha anza na
anaendelea na mwenendo wa kuruhusu askari wengine wajiendeleze kwani faida ya
elimu atakayoipata itamsaidia yeye,jeshi na taifa.
Meja
Yamawe amesema yeyote anaetaka kwenda kusoma amjulishe nay eye atahakikisha
anafanikisha dhamira hiyo ila atakapomaliza lazima alete cheti chake na
asiyeleta cheti atamfungulia mashtaka na kumfukuza jeshi kwani atakuwa amepoteza
fedha za bure za serikali wakati kuna watu wengine wanahitaji huduma kama hiyo.
Hata
hivyo mkuu huyo wa kikosi amesema kuwa licha ya kupata shahada ya pili bado ana
kiu ya kusoma kwani anategemea kusomea shahada ya tatu ya uchumi hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment