Na Senior
Libonge,Kilombero
KUTOPATA fedha kwa wakati
kutoka mfuko wa pamoja(basket fund)na mgawanyo mdogo toka bohari ya madawa
nchini(MSD)ndiko kunakosababisha hospitali ya rufaa ya Mt.Francis iliyopo mjini
Ifakara wilayani Kilombero kupandisha gharama ya matibabu.
Akizungumza katika kikao
cha kamati ya ushauri ya wilaya,mkurugenzi wa hospitali hiyo Dk,Angelo Nyamtema
amesema licha ya kutopata fedha kwa wakati na mgawanyo mdogo pia suala la
ulipaji wa mishahara kwa wataalamu mbalimbali nayo uchangia hospitali hiyo
kukosa fedha.
Dk,Nyamtema amesema licha
ya changamoto hizo alizozitaja mkakati uliopo hivi sasa ni kuboresha huduma
katika hospitali hiyo ili kuweza kufikia hadhi ya hospitali ya rufaa baada ya
kupandishwa hadhi.
Amesema ni mwezi wa tano hivi sasa hawajapata
fedha ya basket fund huku pia wakiwa hawajapata fedha toka serikalini tokea
mwezi Julai mwaka huu ili kuweza kuagiza madawa na vifaa mbalimbali vya tiba
kutoka bohari ya madawa nchini(MSD).
Mkurugenzi huyo wa hospitali ameiomba halmashauri
ya wilaya na serikali kiujumla kushirikiana nao ili kutatua changamoto
zinazowakabili hatimaye kuweza kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi wanaotumia
hospitali hiyo kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Amesema suala la mishahara limekuwa tatizo kwani
kwa kipindi cha karibuni wametumia kiasi cha shilingi milioni 42 kwa ajili ya
kulipa mishahara watumishi wake na fedha hizo zimetokana na fedha zinazotokana
na gharama za uchangiaji zinazotozwa kwa wagonjwa.
Dk,Nyamtema ameiomba serikali kuwapatia wataalamu
walioajiriwa na serikali ili wao waweze kupunguza mzigo mkubwa wa kuwalipa
mishahara na hali hiyo itapelekea kupunguza gharama kwa wananchi wanaopata
huduma katika hospitali hiyo.
Hata hivyo mkurugenzi huyo amekanusha taarifa kuwa
menejimenti ya hospitali uamua kupandisha gharama za matibabu wanapojisikia na
kusema kuwa mawazo ya kupandisha gharama za matibabu sio ufanywa na uongozi wa
hospitali bali ni kamati nzima inayowashirikisha watu kutoka
serikalini,halmashauri ya wilaya na wadau mbalimbali.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kilombero
aliuagiza uongozi wa halmashauri ya wilaya chini ya mwenyekiti wake na
mkurugenzi mtendaji kukaa pamoja na menejimenti ya hospitali hiyo ili kutatua
matatizo mbalimbali hatimaye kuweza kumpunguzia mwananchi mzigo wa gharama za matibabu.
No comments:
Post a Comment