Na
Senior Libonge,Kilombero
MWENYEKITI wa Chama cha
Mapinduzi(CCM) mkoa wa Morogoro Inocent Kalogeris amesema kuwa atakula nae
sahani moja mwanachama yeyote atakaebainika kuwa ni kinara wa makundi ndani ya
chama hicho.
Kauli
hiyo ameitoa jana wakati akizungumza na wananchi wa mji wa Ifakara katika
mkutano wa hadhara uliofanyika katika kiwanja cha Kiungani wenye lengo la
kuimarisha na kukijenga chama.
Kalogeris
amesema kinachoichafua chama hivi sasa ni makundi yaliyopo ndani ya chama hicho
nayayoendelezwa na wanachama wenye uchu wa madaraka na wao wana kina kila
sababu za kuvunja makundi ndani ya chama kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Amewaagiza
viongozi wa chama hicho kuanzia ngazi ya matawi kuwachunguza wale wote
wanaoendeleza makundi na watakaobainika watimuliwe ndani ya chama hicho nay eye
lengo lake ni kupigana na kuhakikisha kuwa CCM hakiyumbi katika mkoa wa
Morogoro.
Kuhusu
baadhi ya viongozi wa vijiji kutosoma taarifa za mapato na matumizi,mwenyekiti
huyo wa CCM mkoa amewataka wahusika kufuata taratibu za kusoma
taarifa hizo na atakaeshindwa kufuata taratibu hatua za kisheria zichukuliwe
dhidi yake.
Aidha
Kalogeris alizungumzia zoezi la uondoaji mifugo katika bonde la Kilombero na
kusema kuwa lengo la zoezi hilo ni kulinusuru bonde hilo na kutaka dola ifanye
kazi yake bila kuhofia mtu na serikali ihakikishe inawapatia maeneo mbadala
wale wote wananchi waliokuwa wakifanya shughuli za kilimo katika eneo la Ramsar
ili kuendeleza shughuli zao za kilimo.
Pia
kiongozi huyo alitoa miezi 6 kwa halmashauri ya wilaya kuhakikisha kero ya maji
ya maji katika mji wa Ifakara inakwisha na pia kutoa miezi 9 kwa halmashauri
hiyo kufanikisha mpango wa wilaya kuwa na hospitali ya wilaya.
Awali
mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala alitaja miradi mbalimbali ambayo
imetekelezwa kama ilani ya chama hicho na kikubwa zaidi kukanusha upotoshaji
unaofanyika juu ya operesheni ya okoa bonde la Kilombero.
Masala
amesema mpaka sasa ni mifugo laki 3 imeondolewa toka zoezi hilo lianze na
linazingatia sheria na kusema kuwa wapo viongozi wanaoendesha kampeni za
kupotosha wananchi wasiondoe mifugo na kusema kuwa wao hawatawaachia viongozi
hao.
Amesema
athari za kuwepo mifugo kwenye bonde hilo ni kubwa na wameongeza wiki 2na
mwisho itakuwa Disema 24 mwaka huu ili kupitia upya kila eneo ili kukagua tena
mifugo na hivi karibuni watatumia tena Helkopta katika ukamilishaji wa zoezi
hilo.
Hata
hivyo Masala alibainisha kuwa hata kama mifugo inayoendelea kukamatwa hivi sasa
ikibainika kuwa ya kiongozi Fulani wao hawatasita kuikamata na kuipiga faini
nay eye atakaechukizwa aende popote nayeye yupo tayari kupambana nae kwani yeye
anafuata sheria bali hafanyi kazi ya kuropoka kwenye vyombo vya habari.
No comments:
Post a Comment