Henry Bernard Mwakifuna,
Ifakara-Kilombero.
Serikali
imeahidi kwa dhati kabisa kusimamia Sheria za Uhifadhi wa Misitu .
Akifunga
Warsha ya Siku Moja ya Uwasilishaji wa Hali Halisi ya Hifadhi ya Misitu ya
Udzungwa, Bi Hawa Mposi Lumuli, Afisa Tarafa ya Ifakara amesema kwa Watumishi
wa Idara ya Misitu wanaolegalega na kutosimamia ipasavyo Sheria, Kanuni na
Taratibu na kukiuka maadili watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Amesema
kuwa tegemeo kubwa la Serikali ni kuona wafanyakazi wa Idara hiyo wanazingatia
maadili na kusaidia kuokoa, kuhifadhi na kutunza misitu.
Kwa
upande wao watafiti kutoka Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania(TFCG)
wamesema kuwa Hifadhi ya Milima ya Udzungwa imeonekana ya Kipekee kwa Uhifadhi
wa Wanyama muhimu na Adimu kama Swala waitwao Vinde na Vyura wa Kihansi.
Vinde, aina ya Swala adimu Misitu ya Asili ya Udzungwa. |
Akiwasilisha
Matokeo ya Utafiti wa Hali ya Msitu wa Udzungwa, Bwana Justine Gwegine ,Afisa
Mtafiti na Mtathimini wa Hali ya Misitu
kutoka Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania(TFCG) amesema kuwa Matokeo ya
ya utafiti wao yameorodhesha Jumla
ya aina za ndege 79 zilionekana na katika maeneo ya Ikule, Chita Wilayani Kilombero na Illutila
na Idegenda katika Wilaya ya Kilolo.
Amesema
kuwa kati ya aina 79 zilizoorodheshwa, aina 14 ambayo
ni asilimia 17 ni wale ndege adimu na pengine wanapatikana katika tao la
mashariki pekee.
Mbega mweupe, kiumbe adimu anyepatikana katika msitu wa Udzungwa |
Lengo la Uwasilishaji
huo ni kufahamu hali ya Misitu na Bioanuai yake kwa ujumla ili kuisaidia
Serikali Kupanga Mipango ya Kuisimamia Vizuri kutokana na Matokeo ya Tafiti.
Utafiti huo umefanyika
kwa Siku 25 Mwezi Septemba na Oktoba mwaka jana ambapo Vijiji Vinne vya Wilaya
za Kilolo na Kilombero zimehusika.
Msitu wa Hifadhi Asili
wa Udzungwa wenye ukubwa wa Hekta 20,720 na ulianzishwa Mwaka 1929,
unasimamiwa na Wakala wa Misitu Tanzania.
No comments:
Post a Comment