Na Senior Libonge- Ifakara
JUMLA ya shilingi milioni 212,886,000 zimepatikana
ikiwa ni mapato ya uwekaji alama mifugo na faini katika zoezi la uondoaji
mifuko katika bonde tengefu la Kilombero kwa wilaya ya Kilombero.
Akizungumza jana katika kikao cha kamati ya
uashauri ya wilaya(DCC)Mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala amesema kuwa
fedha hizo zimepatikana baada ya kuanza kwa zoezi la uwekaji alama lilianza
Agosti 21 na kumalizika Septemba 30 mwaka huu na pia zoezi la faini kwa
wafugaji waliokaidi amri halali lililoanza Oktoba 30 mwaka huu.
Masala amesema zoezi la kuweka alama mifugo
inayostahili kubaki kulingana na ukubwa wa eneo husika lilihusisha vijiji
vilivyopo ndani ya eneo la Ramsar na vilevile nje ya eneo hilo kwa kufanya
mikutano mikuu ya hadhara kwa ajili ya utambuzi wa wafugaji halali na
wanaotakiwa kubaki katika kila kijiji.
Alisema jumla ya ng’ombe 52,780 waliwekwa alama
kwa gharama ya shilingi 1000 kwa kila ng’ombe na kupata jumla ya shilingi
milioni 52,780,000 kama makusanyo ya zoezi hilo na kati ya hizo shilingi
milioni 27,940,300 zilitumika kuendelea na zoezi hilo.
Amebainisha kuwa katika zoezi la uondoaji wa
mifugo ambalo zoezi hilo bado linaendelea mpaka sasa jumla ya wafugaji 2,428
wenye ng’ombe wapatao 9,248 walitozwa faini kwa viwango mbalimbali kulingana na
makosa waliyopatikana nayo.
Mkuu huyo wa wilaya amesema jumla ya ng’ombe 3,482
walitozwa shilingi 10,000 na kupatikana shilingi milioni 34.8 huku ng’ombe
5,379 walitozwa shilingi 20,000 na kupatikana shilingi milioni 107.5,ng’ombe
264 walitozwa shilingi 40,000 na kupatikana shilingi milioni 10.5 na hiyo inafanya
shilingi milioni 152.9 kuwa jumla ya mapato yaliyotokana na faini.
Masala amesema hata hivyo zoezi utoaji wa vibali
vya kusafiria lilienda sambamba na zoezi hilo ambapo idadi ya ng’ombe 4764
walipatiwa vibali kwa gharama ya shilingi 1500 na shilingi milioni 7.1
zimekusanywa kama ruzuku ya serikali kuu.
Amesema fedha zilizoidhinishwa katika zoezi la
uwekaji wa alama ng’ombe na uondoaji wa mifugo katika bonde tengefu la
Kilombero ni shilingi milioni 152.7 na fedha iliyotumika hadi sasa ni shilingi
milioni 94 na kufanya salio la shilingi milioni 14.1.
Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya amesema zoezi la
kuondoa mifugo linaendelea japokuwa linakabiliana na changamoto mbalimbali
ambazo wataalamu wanaendelea kukabiliana nazo
No comments:
Post a Comment