......TUNALENGA Kujenga uwezo wa jamii kushiriki katika utawala na kuwajibisha viongozi wao, kuwezesha jamii kufuatilia matumizi ya fedha za umma kupitia PETS, kutoa elimu ya ardhi na utatuzi wa migogoro ya ardhi, utunzaji wa mazingira, kukuza kipato cha jamii hasa wanawake kupitia VICOBA na kuwawezesha wanafunzi kwa kurahisisha upatikanaji wa vitabu katika vituo vya elimu (student centres) PAMOJA TUNAWEZA......TUSHIRIKIANE..
photos
Welcome to UCRC
About Me
- Ulanga Community Resource Centre
- Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.
Monday, December 31, 2012
TANZIA- MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero afariki dunia
Na Senior
Libonge,Kilombero
MWENYEKITI
wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero Ramadhani Kiombile amefariki katika
hospitali ya taifa ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Taarifa
ambazo zimethibitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero
Jackson Mpankuli zimesema kwamba Kiombile amefariki jana (leo) saa 6 mchana
katika hospitali ya Taifa Muhimbili.
Mpankuli
alisema Mwenyekiti huyo alikuwa anaumwa huku akikataa kueleza ugongwa uliokuwa
ukimsumbua na kwamba sababu zilizopelekea kifo chake zitaelezwa baadaye
baada ya madaktari wa hospitali hiyo kuufanyia uchunguzi mwili huo.
Taarifa
za kifo cha mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero kimestua wakazi
wengi wa wilaya hiyo ambao wengi wao wamekaa katika makundi makundi na
wakijadili baada ya kupata taarifa hiyo huku wengi wao wakiwa hawaamini.
Baada
ya kupata taarifa za msiba huo kila mwananchi wa wilaya ya Kilombero amekuwa
akimpigia simu mwenzie ili kupata ukweli wa kifo hicho na baada ya kupatwa
ukweli kila mmoja amekuwa na majonzi hasa kutokana na uwajibikaji wa mwenyekiti
huyo kijana.
Marehemu
Kiombile licha ya kuwa mwenyekiti wa kwanza mdogo kuongoza
halmashauri hiyo pia alikuwa diwani wa kata ya Ifakara kupitia tiketi ya Chama
cha Mapinduzi(CCM).
Atakumbukwa
kwa mengi hasa ushirikiano kati yake na vijana katika kata yake na wilaya yote
kiujumla pia msimamo wake ambapo alikuwa ahofii kumwambia mtu ukweli pale
anapopata taarifa fulani ambayo inataka kurudisha nyumba maendeleo ya wilaya ya
Kilombero.
Pia
Kiombile anaheshimiwa baada ya kusimamia utengenezaji wa barabara za mitaa ya
kata nzima ya Ifakara ambayo kwa hivi sasa zinapitika kwa msimu mzima na pia
zinarahisisha mgeni yeyote anaeingia katika mji mdogo wa Ifakara kufika popote
atakapo punde atakapoulizia.
Licha
ya hayo pia marehemu alikuwa akisaidia watu wa aina mbalimbali wanaofika katika
ofisi yake wakihitaji msaada wa fedha kwa ajili ya matibabu,shule na shida
mbalimbali ambapo yeye alitoa fedha zake mfukoni na kuweza kuwasaidia.
Wakizungumza
na gazeti hili wakazi wa mji wa Ifakara wamesema kuwa wilaya imempoteza kijana
mchapakazi ambaye uwezo wake ulikuwa unahitajika zaidi hasa baada ya kufanya
mambo makubwa punde alipopata vyeo hivyo vya uwenyekiti na udiwani.
Hiyari
Bohari mkazi wa Ifakara amesema yeye baada ya kupata taarifa ilibidi akae kimya
na kutoamini hasa kutokana na ukaribu alionao kati yake na mwenyekiti huyo hata
kabla hajawa diwani na nafasi ya uwenyekiti.
“Unajuwa
huwezi amini unapopata taarifa za ghafla kama hizi hasa kutokana na ukaribu wa
mtu mwenyewe kwani marehemu nilikuwa nae karibu sana wakati tukiwa pamoja
katika shughuli za usambazaji wa pembejeo na yeye kusema kuwa anaamua kuingia
katika siasa na kweli dhamira yake ilifanikiwa kwa kupata udiwani na
uwenyekiti,”alisema Hiyari.
Naye
John Torogo mkazi wa Kidatu wilayani hapa alisema kuwa kifo cha Kiombile ni
pigo kwa vijana wote wa wilaya hiyo kwani alikuwa mpiganaji wa kweli bila
kuhofia mtu wala chama kwani alikuwa akisimamia haki katika kutatua matatizo
mbalimbali ya wananchi katika wilaya ya Kilombero.
Kwa
upande wake makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo David Ligazio alisema kuwa
aamini mwenyekiti wake amefariki dunia kwani mara kwa mara alikuwa akiwasiliana
na mtu wa karibu aliyekuwa akimuhudumia na kumuelezea kuwa afya yake inaimarika
ila alipopigiwa simu na kaimu mkurugenzi pamoja na mkuu wa wilaya nguvu zote
zilimuishia.
Naye
mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilombero Abdallah Kambangwa amesema kuwa naye
ameshtushwa na habari za msiba huo kwani marehemu alikuwa akishirikiana nae
vizuri ndani ya kazi za chama na za nje ya chama akimchukulia kuwa ni mdogo
wake hivyo asingekubali apotosheke wakati yeye yupo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment