HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Sunday, January 6, 2013

HALMASHAURI YA WILAYA YA ULANGA YALIPA MADENI HOSPITALI YA LUGALA


Na Senior Libonge, Ulanga

Halmashauri ya wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, hatimaye imeanza kulipa madeni iliyokuwa ikidaiwa na hospitali ya Lugala iliyoko katika tarafa ya Malinyi wilayani humo baada ya kupata fedha zinazotokana na makusanyo ya ndani ya halmashauri hiyo.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Furaha Lilongeri, halmashauri hiyo tayari imeandaa malipo ya zaidi ya Sh40 milioni kwa ajili ya kuilipa hospitali ya Lugala baada ya hospitali hiyo kutoa huduma ya bure kwa akinamama wajawazito na watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano.

Alisema kuwa halmashauri yake mwaka jana ilisaini mkataba na uongozi wa hospitali ya Lugala ili kuweza kutoa huduma bure kwa makundi hayo huku fedha za kulipia gharama hizo zikipangwa kupatikana na mfuko wa pamoja wa serikali kuu na mapato ya ndani ya nchi.

Hata hivyo, tathimini iliyofanywa na halmashauri ya wilaya ya Ulanga katika kipindi cha miaka mitatu ya utekelezaji wa mkataba huo kuanzia Julai mpaka Septemba 2012, halmashauri hiyo ilikuwa ikidaiwa jumla ya Sh62.1 milioni.

Lilongeri alisema kuwa kwa mujibu wa takwimu hizo, ilibainika pia kuwa idadi ya wagonjwa waliokuwa wakitarajiwa kutibiwa katika hospitali hiyo kupitia mkataba huo iliongezeka mara dufu kiasi cha kutishia bajeti ya halmashauri hiyo.

Aliongeza kuwa uchanganuzi uliofanywa na halmashauri hiyo ulionyesha kuwa idadi ya wagonjwa wanaotibiwa katika hospitali hiyo huenda ikaongezeka zaidi na kulifanya deni la halmashauri kupanda na kufikia wastani wa zaidi ya Sh248 milioni kwa kipindi cha mwaka mmoja wa utekelezaji wa mkataba huo.

Mwenye kiti huyo alidai kuwa kama jinsi ambavyo halmashauri ilivyoadhimia na kuuomba uongozi wa halmashauri hiyo kufanya mazungumzo ya kulekebisha mkataba huo na kuufanya makata huo kuuruhusu wagonjwa kutibiwa baadhi ya magonjwa hususan watoto wenye umri wa miaka mitano na akinamama wajawazito na magonjwa mengine kutibiwa katika zahanati za serikali zilizopo.

“Tumekwisha andaa malipo ya hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya deni tunalodaiwa na baada ya kuwakabidhi fedha zao tutaomba maongezi yaweze kufanyika ili kuruhusu mkataba huo kufanyiwa marekebisho.



No comments:

Post a Comment