HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, October 11, 2012

Umaskini katikati ya msitu wa ndizi mbingu.



Na Rwambogo Edson

Kata ya Mbingu ipo kusini mwa wilaya ya kilombero. wilaya hiyo inaunda jimbo moja la uchaguzi ambalo ni jimbo la kilombero mkoani Morogoro. Mkoa wa morogoro una ukubwa wa kilometa za mraba 70,799. Kata ya mbingu ipo kilometa 290 kutoka Morogoro mjini, mji ambao ni makao makuu ya mkoa. Umbali kutoka makao makuu ya wilaya Ifakara ni kilometa 60. Kijiografia upande wa magharibi na kaskazini kata ya mbingu imepakana na hifadhi ya Milima ya Udzungwa. Sehemu kubwa ya kata hii ni tambalale na baadhi ya vijiji vipo milimani.

Wakazi wa kijiji cha Mbingu ni wakulima wa ndizi maarufu kwa jina la ndizi Mzuzu. Pamoja na zao hilo kustawishwa kwa wingi katika maeneo mengi ya wilaya ya kilombero ikiwemo Mbingu, lakini pia mazao kama Cocoa, mahindi, mpunga, miwa na mazao mengine pia hustawishwa kwa wingi katika kijiji hiki. Mzee madeje anasema ata jina mbingu inasemekana lilitokana na kuwa kila kitu kinacholimwa mbingu kinastawi pamoja na umbali uliopo kutoka miji mingine.

Mwenyekiti wa kijiji cha Mpofu Bwana John Haule John anasema kata ya mbingu imegawanyika sehemu za milimani na mabondeni. Wanakijiji cha mpofu kilichopo uwanda wa milimani hutegemea zaidi kilimo cha ndizi, wananchi hao hulima kwa mwaka mzima zao hilo ata wakati wa masika. Tofauti na Wakazi wa vijiji vya mabondeni wakati wa masika hulima kilimo mseto zaidi kwa kuchanganya kilimo cha mpunga, mahindi, maharagwe na mazao mengine.

Bwana haule anaongeza kuwa wakati wa masika biashara ya ndizi kwa upande wa vijiji vya milimani huwa nzuri kwani bei ya ndizi hupanda kidogo. Mkungu mmoja huanzia bei ya shilingi mia nane kwa mikungu midogo maarufu kwa jina la viserebende mpaka elfu tano kwa mkungu mkubwa. Lakini wakati wa kiangazi mkungu mdogo huuzwa kwa shilingi mia mbili mpaka mia tano na wakati mwingine hutolewa kama nyongeza kwa wafanya biashara wakubwa.

Kijana Harrison Makaye mwanafunzi mkazi wa kijiji cha mpofu aliyehitimu masomo ya mawasiliano ya umma mwaka huu anasema, wakati wa masika biashara huwa ngumu zaidi kwa kuwa magari mengi kama fuso hayafiki kutokana na sehemu iliyopo barabara kuu kutoka makao makuu ya wilaya Ifakara ipo sehemu ya bonde, kutokana na mafuriko ya mto Lwipa barabara hujaa maji baadhi ya sehemu korofi.

Anasema hali hiyo huwalazimu wakulima kusafirisha ndizi kwa usafiri wa baiskeli mpaka kijiji cha Namawala ambapo magari kutoka sehemu mbalimbali huishia. Lakini pia walanguzi hutumia nafasi hiyo kuwa kandamiza wakulima kwa kuwapangia bei wanazozitaka kwani umbali kutoka mbingu mpaka Namawala ni zaidi ya kilometa kumi na tano kwa hiyo wakulima hawawezi kurudi na mzigo majumbani mwao kutokana na umbali huo. Wakati mwingine wakulima hulazimika kutupa ndizi wanazoshindwa kupata soko lake huko wanakopereka .

Wanakijiji cha mbingu, pamoja na kuwa na utajiri wa ardhi inayokubali kustawisha kila aina ya zao, lakini bado hawana shule za msingi za uwakika. Mwanafunzi Filbert Madeje anasema inatokana na wazazi wao kuwa na kipato kidogo na kisicho cha uwakika katika kuchangia maendeleo ya shule. Mfano wananfunzi wa Shule ya Msingi Mpofu wanasomea chini ya Mti na wengine katika madarasa yaliyoezekwa kwa nyasi bila kuzibwa pembeni. Mzee hamisi mfanya biashara na mlanguzi wa ndizi kwa kipindi kirefu anasema inatokana na serikali kutokuongeza idadi ya majengo kulingana na ongezeko la watu.

Mzee Hamis Anasema wakati wanaanza biashara ya ndizi hapakuwa na watu wengi kama ilivyo sasa. Anasema ata vituo vya Polisi kwa ajiri ya usalama wa raia pia havijaongezwa, hospiatali ipo moja nayo muda wote haina madawa ya kutosha. Barabara nayo inaharibika bila kufanyiwa marekebisho, mfano daraja ambalo ni kiunganishi kati ya kijiji cha mpofu na Londo ni bovu na tangu lilipojengwa kwa nguvu za wananchi miaka mitano iliyopita limebaki lile lile la mbao ambalo linahatarisha wanaolitumia na halina uwezo wa kupitisha vyombo vya usafiri zaidi ya baiskeri.

Mradi wa Soko la pamoja la ndizi lililotarajiwa kujengwa kwa ajiri ya wakulima wadogo umebakia historia tangu lilipoanza kujengwa na kuishia kwenye msingi, imepita miaka minne bila kumaliziwa.

Kuhusu usafiri wa reli ya Uhuru mkulima wa ndizi kijiji cha Londo Bwana Philimoni Mgogo anasema, ufanisi mdogo wa reli ya Uhuru umewaathiri, hasa ikizingatiwa miaka ya tisini wakulima walikuwa wakiuza ndizi nyingi sana kwa kuwa wateja wao walikuwa wanabeba mzigo mkubwa kupitia usafiri wa reli. Anasema usafiri wa reli haukuwa wa msimu ata wakati wa masika hawakuwahi kuwaza wangeuza wapi ndizi zao.

Nae mzee kondo anaongeza kwa kusema wafanya biashara wa Mbingu walikuwa wanabeba ndizi zao mpaka Dar es salaam na kuuzia steshen ya TAZARA. Anasema wakati mwingine walikuwa wakimaliza mzigo kabla hawajafika Dar es salaam na kugeuza wakiwa na hera ya kulipia watoto karo. Anasema hawakuwa ombaomba kama walivyo sasa kwa kuwa usafiri wa Reli sasa hivi hauna uwakika. Mfano unaweza ukaambiwa treni itapita saa tano asubuhi ikapita saa tano usiku, hali hiyo inawakatisha tamaa wafanya biashara wadogo hasa ikizingatiwa hawana vifaa vya kuhifadhia bidhaa zisiharibike .

Wakulima wa kijiji cha mbingu wanasema usafiri wa kutegemea magari unawaumiza, kwa sababu mafuta yakipanda ghalama za usafiri zinapanda pia. Lakini ghalama za ndizi zinabaki pale pale, pia magari yanasafirisha ndizi msimu wa kiangazi tu, wakati wa masika magari hayafiki, ata kipindi cha kiangazi ndizi huwa nyingi zaidi hali inayoperekea ndizi zinaendelea kubaki na wakati mwingine zinaoza.

Kuhusu mafuriko yaliyotokea mwezi wa nne mwaka huu, Afsa Mtendaji wa kijiji cha Mpofu bwana Charles Tapule anasema wananchi wengi wameathirika kutokana na mafuriko hayo. Kuna baadhi wamefiwa na mifugo yao, hifadhi ya chakula iriharibika na baadhi ya maeneo miundo mbinu iliharibiaka kabisa.

Lakini anawashukuru wahisani na Serikali kwa kujitolea mavazi pamoja na vyakula kwa ajiri ya wahanga wa tukio hilo. Pia anawaomba wakazi wa kijiji hicho kutumia misimu ya mvua vizuri inayokuja kuweka hifadhi ya chakula na kujenga vizuri makazi yao kwa ajiri ya kujikinga na hali hiyo. Wanakijiji wa kijiji cha Londo na maeneo mengine katika kata ya Mbingu waliathirika na mafuriko yaliyotokana na mvua za masika zilizonyesha mwezi wa nne mwaka huu.

Lakini pamoja na hayo, Bwna tapule anatoa wito kwa Serikali kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi jinsi ya kutumia Mbolea za ruzuku. Hali hiyo inatokana na wananchi wengi kutoitikia mwito wa kutumia Mbolea kwenye mashamba ya Ndizi, kwa madai mbolea za viwandani zinaua rutuba ya ardhi na kusababisha baadhi ya mazao ya asili kutoweka.

Kauli hiyo inathibitishwa na Mzee Madeje, ambaye anasema ni kweli mazao mengi ya asili yametoweka baada ya wananchi kuanza kutumia Mbolea za viwandani. Mfano wa mazao hayo ni kama vile mbogamboga kama mchicha poli, Nyanya poli, mapera, mapensheni poli, mchunga, mnavu na mengine mengi. Anaongeza kwa kusema ata magonjwa ya mazao yamekuwa mengi sana kwani ata minazi na ndizi vinashambuliwa siku hizi.

Kuelekea miaka hamsini ya Uhuru mwenyekiti wa kijiji cha Mpofu anatoa wito kwa serikali kuliangalia upya suala la usafiri wa reli na kuiomba irudishe ufanisi wake kama zamani. Anasema alama ya wananchi wa mkoa wa Morogoro kuwa walipata uhuru ni ufanisi bora wa reli ya Uhuru. Anasema ata baadhi ya wanakijiji wanarazimika kuanza kukimbilia kulima mazao wasiyoyajua kama Cocoa kutokana na soko la ndizi kuendelea kudorola kila kukicha kutokana na ugumu wa usafiri.

nao baadhi ya wanakijiji wameanza kukata na kuchimbua migomba kama walivyofanya wananchi wa maeneo ya kilombero baada ya kuchimbua michungwa na kulima miwa. Uongozi na serikali umeanza kuwahamasisha wananchi wa Mbingu kulima miwa kwa ajiri ya kiwanda cha sukari cha kilombero.

Mfanya biashara ndogondogo Bi Magreti Benjamini anasema suala hilo lisipoangaliawa vizuri wananchi wengi watakipuuza kulimo cha ndizi na watageukia kwenye mazao ya Cocoa na Miwa. Kwa sababu wanunuzi wa miwa na cocoa wananunua kwa bei nzuri na hawasumbui. Anasema imefikia wakati baadhi ya walanguzi kutoka Dar es salaam wanawakopa wakulima wa ndizi, na kutokomea na hera zao wanazowadai wafanyabiashara wa Mbingu

No comments:

Post a Comment