HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Wednesday, October 31, 2012

IDADI KUBWA YA WANYAMA YATOWEKA BONDE LA KILOMBERO


Henry Bernard Mwakifuna, Itete-Ulanga

UVAMIZI wa Makazi, Kilimo na Mifugo ni sababu kubwa zinazopelekea kutoweka kwa baadhi ya Wanyama katika Hifadhi ya Bonde Tengefu la Kilombero.

Bwana Hassan Masala, Mkuu wa Wailaya ya Kilombero akisoma Risala ya Hali Halisi ya Bonde Tengefu la Kilombero katika uzinduzi wa Operesheni Okoa Bonde la Kilombero iliyofanyika hii leo Tarehe 30/10/2012 katika Kata ya Itete Wilayani Ulanga amesema kuwa Wanyama waliokuwapo katika Bonde hilo wamepungua kwa asilimia kubwa .

Amesema kuwa kulikuwa na Nyati 35,301 Mwaka 1991 lakini Mwaka 2009 Sensa ya Wanyama hao imebakia ni 1462 ni asilimia 4 tu ya wanyama hao, Mwaka 1991 kulikuwa na Tembo 1848 lakini Sensa ya Mwaka 2009 wamebakia Tembo 1,535.

Wakati Wanyama adimu aina ya Sheshe ambao ni jamii ya wanyama wanaopatikana sehemu 18 tu Duniani ikiwemo Kilombero wamebakia 18,161 Mwaka 2009 kutoka 36,569 Mwaka 1991 kwa muujibu wa Takwimu zilizofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyama Pori nchini (TAWIRI).


Bonde Tengefu la Kilombero ni Makazi ya Asilimia 75 ya Sheshe wote wanaopatikana Duniani na Wito umetolewa kuweza kuwalinda wanyama hao wanaotoweka kwa kasi Ulimwenguni.

Operesheni Okoa Bonde la Kilombero imezinduliwa leo na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwana Said Mecky Sadiq, ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment