HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, October 11, 2012

MIFUGO ZAIDI YA 20 YAFA KWA KUKOSA MAJI NAMHANGA

Henry Bernard Mwakifuna, Namhanga Ulanga
 
ZAIDI ya Ngombe na Mbuzi 20 wamekufa kwa kukosa maji katika Kitongoji cha Mbenja, kijiji cha Namuhanga Wilayani Ulanga.
 
Nkuba Ngwandu, Mwenyekiti wa Kikundi cha Wafugaji cha Mbenja Livestock cooperative amesema Mifugo hiyo imekufa kutokan na  Serikali Wilayani Ulanga kukataza kunywesha Maji mifugo yao katika Mto Mnjeta.
 
Mbali ya Tatizo hilo Wafugaji hao wamelalamikia Mipaka iliyowekwa na Serikali kuwa ipo ndani ya makazi yao.
 
Baadhi ya Wafugaji wamesema kuwa  wameingia katia eneo  la Mbenja kihalali baada ya kuomba maombi yao kwa serikali ya kijiji cha Namuhanga na kukubaliwa kuishi katika eneo hilo.
 
Mwenyekiti wa kijiji cha Namuhanga Bwana Iddi Lihogoya amekiri serikali kuwakataza Wafugaji kunywesha  mifugo kyao katika Mto Mnjeta na Kuongeza kuwa Wafugaji hao wameingia kihalali katika kijiji hicho baada ya kuandika barua ya kuomba kuishi katika eneo la Mbenja na wananchi wa kijiji hicho kukubali.
 
Kwa upande wake Bwana Francis Miti , Mkuu wa Wilaya ya Ulanga amekiri Serikali kuwakataza Jamii ya Wafugaji wa eneo la Mbenja, kunywesha Mifugo yao katika Mto Mnjeta kwa kuwa tayari Maeneo hayo yapo katika Eneo la Hifadhi ambapo Shughuli zozote za Kuichumi ikiwa pamoja na Ufugaji  hairuhusiwi kuingia katika Eneo hilo.
 
Amewataka Wafugaji kuchimba Mabwawa ya kunyweshea mifugo yao ili kuokoa mifugo yao inayokufa kwa kukosa maji ambapo hapo awali wamekuwa wakitegemea kunywesha mifugo yao katika mto mnjetwa.
 
Amesema wafugaji wajitokeze kuchimba mabwawa ya maji na serikali inaweza kuwasaidia katika kuchimba mabwawa ya maji baada ya nguvu zao kuonyesha kwanza.

No comments:

Post a Comment