HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, October 11, 2012

Upungufu wa Maji unatisha mto Kilombero

Na Ferdinand Nachenga

Jana nilipata bahati ya kutembelea kivuko cha Mto Kilombero maarufu kama kivukoni mida ya saa kumi na mbili jioni. Nikakaa kwenye pub ya upande wa Ifakara japo ilikua inanuka maana kuna choo kisichosafichwa kwa muda mrefu karibu na hiyo pub.

Hapakua na watu,nikaagiza kinywaji kisha nikapanda juu na kuanza kuangalia mandhari ya bonde la Kilombero. Nilichoshuhudia ni jinsi gani kilimo na ufugaji vilivyoathiri mto kilombero. Sijawahi kuona maji ya mto huu kukauka kiasi kile,nadhani ulimaji karibu kabisa na mto pamoja na ufugaji inabidi vipigwe vita sana ili kunusuru mto huu na bonde kwa ujumla.

Pantoni lilikua linaendelea na shughuri zake japo wanasema mwisho saa kumi na mbili jioni. cha ajabu ni kwamba pantoni haina taa inatumia taa za magari yanayopakiwa humo dah nilisikitika sana huku niki...kumbuka kilichotokea miaka kadhaa iliyopita.

Kufika saa mbili hivi nikashuka chini na kuona mlinzi anazuia watu wasiingie maana muda umeisha lakini kama una 500 unaruhusiwa na pikipiki ni 2000 bila kutoa risiti. Nami nikajifanya nataka kuvuka lakini jamaa alisema bila 500 nisubiri kesho na mia mbili yangu.

Wenye pesa walienda na wengi masikini walikwama hasa wakina mama. Nilipouliza kwa nini wanafanya hivyo nikaambiwa wao wakale wapi? kwa hiyo zile zote ni zao. Niliumia sana lakini huo ndio uozo wa uongozi wa wilaya yetu. yani hata taa ya pantoni hawawezi kununua? Ajali ikitokea nani alaumiwe? nani atafidia wahanga?kwa gharama ipi? ..we need to act now guys....

No comments:

Post a Comment