HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Sunday, October 21, 2012

Ulanga yapania kuboresha huduma za Afya

Na Senior Libonge,Ulanga
HALMASHAURI ya wilaya ya Ulanga imeiomba serikali itoe kipaumbele kwa hospitali ya wilaya hiyo ili iweze kukamilisha ukarabati wa majengo yake ambayo hayakidhi mahitaji halisi ya wananchi wa wilaya hiyo.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa wodi ya kisasa ya wazazi katika hospitali hiyo mganga mkuu wa wilaya ya Ulanga Dk Jacob Frank amesema majengo yaliyopo hivi sasa ni ya zamani na hayakidhi mahitaji halisi hivyo ukarabati wake utaboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Dk Frank ameamua kutoa ombi hilo baada ya serikali kuikabidhi hospitali hiyo asilimia 30 tu ya fedha yote inayohitajika kwa ajili ya ukarabati huo tangu mwaka 2007/2008 ambayo ni shilingi milioni 600 wakati hospitali hiyo ilitengewa kiasi cha shilingi bilioni 2.
Amesema licha ya changamoto ya uchakavu wa majengo pia wanatatizo la upungufu wa watumishi wenye ujuzi,kukosekana kwa gari la kubebea wagonjwa,upungufu wa madawa na vitendea kazi na uchakavu wa majengo.
Hata hivyo mganga mkuu huyo amesema kwa hivi sasa matarajio yao ni kuendelea kuomba nafasi za kuajiri watumishi wenye ujuzi wa kada mbalimbali,kuongeza bajeti ya kununulia madawa na vitendea kazi kutoka vyanzo mbalimbali kana CHF,NHIF na Basket Fund ili kukidhi mahitaji halisi na kuendelea kuomba fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa hospitali.
Ameishukuru serikali pamoja na wafadhili wao wa Afya taasisi ya World Lung Foundation kwa misaada wanayipata katika kuboresha huduma za mama na mtoto wilayani humo.
Mganga mkuu huyo amesema kuwa taasisi ya World Lung Foundation licha ya kuwatengenezea wodi ya upasuaji kwa ajinamama pia wameviongezea hadhi vituo vya afya vya Mtimbira na Mwaya ambavyo vimeshaanza kutoa huduma za upasuaji na pia wanatoa mafunzo kwa watumishi wa kada mbalimbali ambao hufanya shughuli za upasuaji na utoaji wa dawa za usingizi kwenye vyumba vya upasuaji.
Kwa upande wake meneja mradi wa World Lung Foundation Dismas Masumbuko amesema kwa awamu hii inayomalizika mwaka 2015 wametenga dola za kimarekani milioni 8.5 lakini fedha zitaongezeka hadi kufikia dola milioni 15.5 punde ikimalizika awamu hii ya kwanza.
Masumbuko amesema toka wafungue vituo vya afya na kutoa mafunzo kwa wataalamu wa afya katika maeneo mbalimbali nchini huduma ya uzalishaji salama wa akinamama umeongezeka toka kinamama 20 hadi kufikia akinamama 120 kwa mwezi na kusema kuwa ili kuboresha zaidi huduma wameanzisha kutoa huduma kwa njia ya teknolojia ya mawasiliano.

No comments:

Post a Comment