HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Wednesday, October 31, 2012

Ifakara wapania kutokomeza uvuvi haramu



Na Senior Libonge,Kilombero

JUMLA ya zana za uvuvi haramu yakiwemo makokoro 35 na nyavu ndogo 4 vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 28.6 zimekamatwa katika doria zilizofanyika katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2012 katika mamlaka ya mji mdogo wa Ifakara.

Kwa mujibu wa afisa mtendaji wa mamlaka ya mji mdogo wa Ifakara Mercy Minja amesema mpaka sasa kesi zilizopelekwa mahakamani ni tano ambazo ni za kukamatwa na kokoro,kutishia kwa njia ya simu baada ya kukamatwa,kumiliki kokoro,kumiliki kokoro na kujeruhi kwa panga baada ya kukamatwa.

Mercy amesema lakini cha kushangaza hakuna mtuhumiwa aliyefungwa hadi sasa licha ya serikali kupitia mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera wakati akifungua miezi ya karibuni kuagiza jeshi la polisi na mahakama kutowachelewesha kuwahukumu wale wote watakaopatikana na hatia ya uvuvi haramu katika mto Kilombero.

Hata hivyo wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo wameiomba halmashauri ya wilaya kusimamia kwa umakini zoezi la doria kwa kushirikiana nao na hatimaye kuhakikisha vyombo vya sheria vinawahukumu haraka iwezekanavyo watuhumiwa ili kuwapa moyo wale wote wanaoendeleza doria katika mto huo.

Aidha mtendaji huyo wa mamlaka ya mji mdogo alizungumzia suala la ujenzi holela katika maeneo mbalimbali ya mamlaka ya mji mdogo Ifakara na kusema kuwa kumekuwepo na uvmizi wa ujenzi wa nyumba za makazi au za biashara katika maeneo hasa ya hifadhi ya barabara.

Amesema ujenzi huo unasababisha kushindikana kuwepo miundombinu ambayo inatakiwa kuwekwa pembezoni mwa barabara na kuitaja kuwa ni mifereji ya maji taka,upitishaji wa mkongo wa mawasiliano wa Taifa na nguzo za umeme.

Mercy amesema pia kumekuwepo na ubadilishaji wa matumizi ya ardhi bila ya kuwa na kibali cha kubadili matumizi ya ardhi hiyo kwa mfano kupewa eneo kwa ajili ya kujenga nyumba ya makazi lakini mtu anabadilisha na kujenga nyumba ya kulala wageni ama kiwanda bila kuwasiliana na mamlaka husika yenye jukumu hilo.

Amewaomba wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo kulisimamia na kuzuia watu kujichukulia sheria mkononi mwao kwa kuwazuia na kuwaelekeza nini cha kufanya ili waweze kuepuka kuendelea kubomolewa nyumba zao walizojenga bila kufuata kanuni,sheria na taratibu za ujenzi katika mamlaka ya mji mdogo.

No comments:

Post a Comment