HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Wednesday, October 17, 2012

ULANGA WAZINDUA WODI YA KISASA YA UPASUAJI KWA WAZAZI



Na Senior Libonge,Ulanga


KATIKA kuboresha huduma za akinamama wajawazito ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto vitokanavyo na madhara wakati wa kujifungua,wilaya ya Ulanga imezindua wodi ya wazazi ya kisasa yenye thamani ya shilingi milioni 205,904,500.
Uzinduzi huo ulifanyika jana katika hospitali ya wilaya mbele ya katibu tawala wa mkoa wa Morogoro Eliya Ntandu ambapo katika uzinduzi mtoto wa kwanza wa kiume alizaliwa baada ya mzazi wake kufanyiwa upasuaji wa kwanza uliokuwa wa mafanikio.

Mtoto wa kwanza kuzaliwa kwa upasuaji baada ya uzinduzi wa wodi hiyo


 Katibu tawala mkoa wa Morogoro Eliya Ntandu akizungumza na wananchi wa mji wa Mahenge wakati wa uzinduzi wa wodi ya kujifungulia akinamana, kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti na kulia kwake ni mwenyekiti wa halmashauri Furaha Lilongeri.

Katibu tawala mkoa wa Morogoro Eliya Ntandu akikata utepe kuashiria uzinduzi wa wodi ya upasuaji kwa akinamamaa katika hospitali ya wilaya ya Ulanga,kushoto ni meneja mradi wa World Lung Foundation Abbas Masumbuko na kulia ni mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti

Kwa mujibu wa mganga mkuu wa wilaya ya Ulanga Dk Jacob Frank amesema mradi wa ujenzi huo ulianza kutekelezwa mwaka 2010 baada ya makubaliano kati ya halmashauri ya wilaya ya Ulanga na shirika la World Lung Foundation kutoka nchini Marekani.
Dk Frank alisema kazi ya ujenzi wa jingo hilo ulitekelezwa kwa awamu mbili kwa awamu ya kwanza kugharimu shilingi milioni 91,395,500 ikiwa ni fedha zilizotolewa na World Lung Foundation na kazi zilizofanyika ni kusafisha eneo,kuchimba na kujenga msingi,kujenga ukuta na kupaua.
Amesema awamu ya pili ilihusisha kazi ya umaliziaji wa ujenzi wa jengo ambapo kiasi cha shilingi milioni 82,192,450 zilitumika ambazo zilitengwa na halmashauri ya wilaya ya Ulanga lakini ilibidi halmashauri hiyo kutumia force account na hadi kukamilika kwa mradi huo halmashauri hiyo imekwisha tumia gharama ya shilingi milioni 114,509,000.
Mganga huyo amesema ili licha ya kugharamia jengo pia wafadhili hao wa World Lung Foundation wametoa vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 45 ikiwemo kitanda cha upasuaji,baby cot,air condition,suction machine,vifaa vya upasuaji,pass oxmiter,mashine ya kutolea dawa ya usingizi na vitanda vya kujifungulia.
Licha ya kuzindua wodi hiyo ya kisasa kujifungulia akinamama wajawazito hospitali hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa watumishi wenye ujuzi hasa madaktari,wauguzi,matabibu na wateknolojia maabara,kukosekana kwa gari la wagonjwa,upungufu wa madawa na vitendea kazi na uchakavu wa majengo.
Kwa upande wake meneja mradi wa World Lung Foundation Dismas Masumbuko amesema kwa awamu hii inayomalizika mwaka 2015 wametenga dola za kimarekani milioni 8.5 lakini fedha zitaongezeka hadi kufikia dola milioni 15.5 punde ikimalizika awamu hii ya kwanza.
Masumbuko amesema toka wafungue vituo vya afya na kutoa mafunzo kwa wataalamu wa afya katika maeneo mbalimbali nchini huduma ya uzalishaji salama wa akinamama umeongezeka toka kinamama 20 hadi kufikia akinamama 120 kwa mwezi na kusema kuwa ili kuboresha zaidi huduma wameanzisha kutoa huduma kwa njia ya teknolojia ya mawasiliano.
Naye mgeni rasmi Katibu tawala mkoa wa Morogoro Eliya Ntandu amewapongeza wafadhili hao kwa kutekeleza malengo yao tofauti na baadhi ya taasisi nyingine ambazo azifuati sera zao.
Ntandu amewataka akinamama wajawazito wilayani humo kwenda kwa wingi kujifungulia katika hospitali ya wilaya na kuacha kujifungulia majumbani hasa baada ya huduma kuboreshwa ila amewataka watumishi wa afya kutumia vyema vifaa walivyopata ili kuokoa vifo vya akinamama na wajawazito.

 

No comments:

Post a Comment