HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, December 17, 2012

JKT Chita wapewa somo


Na Senior Libonge,Kilombero

WITO umetolewa kwa askari wa kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa(JKT Chita) kujiwekea malengo yao hasa katika suala la elimu ili kuweza kutimiza ndoto zao pamoja na za familia zao.

Akizungumza na askari hao katika tafrija ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka mpya sambamba na kumpongeza mkuu wa kikosi hicho Meja Msabaha Yamawe kwa kupata shahada ya pili ya uzamili ya uhasibu na fedha,mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala amesema kuwa moja ya majukumu ya kutimiza malengo yako ni kupata elimu.

Masala amesema kinachofanyika hivi sasa kwa askari nchini ni kubweteka baada ya kupata ajira bila kufahamu kuwa kujiendeleza kwa elimu ni kupiga hatua moja zaidi ya maisha hasa katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia.

Amempongeza mkuu wa kikosi hicho kwa kujiendeleza na kupata shahada ya pili bila kuridhika na mamlaka makubwa ya kuwaongoza wenzie na kusema kuwa kiongozi huyo amekuwa mfano mzuri kwa wenzie hivyo na askari waliopo chini yake pia waige mfano huo.

Masala amemtaka mkuu huyo wa kikosi kunufaisha wenzake kwa elimu aliyoipata na kuwa mfano bora kwa wafanyakazi wenzie na familia yake na hasa kuwaruhusu wale wote wanaotaka kujiendeleza ili mradi wafuate sheria za kijeshi.

Naye meja Yamawe amemuhakikishia mkuu huyo wa wilaya kuwa elimu aliyoipata ataitumia kwa faida ya jeshi na taifa kiujumla na kusema kuwa alikwisha anza na anaendelea na mwenendo wa kuruhusu askari wengine wajiendeleze kwani faida ya elimu atakayoipata itamsaidia yeye,jeshi na taifa.

Meja Yamawe amesema yeyote anaetaka kwenda kusoma amjulishe nay eye atahakikisha anafanikisha dhamira hiyo ila atakapomaliza lazima alete cheti chake na asiyeleta cheti atamfungulia mashtaka na kumfukuza jeshi kwani atakuwa amepoteza fedha za bure za serikali wakati kuna watu wengine wanahitaji huduma kama hiyo.

Hata hivyo mkuu huyo wa kikosi amesema kuwa licha ya kupata shahada ya pili bado ana kiu ya kusoma kwani anategemea kusomea shahada ya tatu ya uchumi hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment