HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, December 17, 2012

CCM Moro wakemea makundi


Na Senior Libonge,Kilombero

MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi(CCM) mkoa wa Morogoro Inocent Kalogeris amesema kuwa atakula nae sahani moja mwanachama yeyote atakaebainika kuwa ni kinara wa makundi ndani ya chama hicho.

Kauli hiyo ameitoa jana wakati akizungumza na wananchi wa mji wa Ifakara katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kiwanja cha Kiungani wenye lengo la kuimarisha na kukijenga chama.

Kalogeris amesema kinachoichafua chama hivi sasa ni makundi yaliyopo ndani ya chama hicho nayayoendelezwa na wanachama wenye uchu wa madaraka na wao wana kina kila sababu za kuvunja makundi ndani ya chama kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2015.

Amewaagiza viongozi wa chama hicho kuanzia ngazi ya matawi kuwachunguza wale wote wanaoendeleza makundi na watakaobainika watimuliwe ndani ya chama hicho nay eye lengo lake ni kupigana na kuhakikisha kuwa CCM hakiyumbi katika mkoa wa Morogoro.

Kuhusu baadhi ya viongozi wa vijiji kutosoma taarifa za mapato na matumizi,mwenyekiti huyo wa CCM mkoa amewataka wahusika kufuata taratibu  za kusoma taarifa hizo na atakaeshindwa kufuata taratibu hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Aidha Kalogeris alizungumzia zoezi la uondoaji mifugo katika bonde la Kilombero na kusema kuwa lengo la zoezi hilo ni kulinusuru bonde hilo na kutaka dola ifanye kazi yake bila kuhofia mtu na serikali ihakikishe inawapatia maeneo mbadala wale wote wananchi waliokuwa wakifanya shughuli za kilimo katika eneo la Ramsar ili kuendeleza shughuli zao za kilimo.

Pia kiongozi huyo alitoa miezi 6 kwa halmashauri ya wilaya kuhakikisha kero ya maji ya maji katika mji wa Ifakara inakwisha na pia kutoa miezi 9 kwa halmashauri hiyo kufanikisha mpango wa wilaya kuwa na hospitali ya wilaya.

Awali mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala alitaja miradi mbalimbali ambayo imetekelezwa kama ilani ya chama hicho na kikubwa zaidi kukanusha upotoshaji unaofanyika juu ya operesheni ya okoa bonde la Kilombero.

Masala amesema mpaka sasa ni mifugo laki 3 imeondolewa toka zoezi hilo lianze na linazingatia sheria na kusema kuwa wapo viongozi wanaoendesha kampeni za kupotosha wananchi wasiondoe mifugo na kusema kuwa wao hawatawaachia viongozi hao.

Amesema athari za kuwepo mifugo kwenye bonde hilo ni kubwa na wameongeza wiki 2na mwisho itakuwa Disema 24 mwaka huu ili kupitia upya kila eneo ili kukagua tena mifugo na hivi karibuni watatumia tena Helkopta katika ukamilishaji wa zoezi hilo.

Hata hivyo Masala alibainisha kuwa hata kama mifugo inayoendelea kukamatwa hivi sasa ikibainika kuwa ya kiongozi Fulani wao hawatasita kuikamata na kuipiga faini nay eye atakaechukizwa aende popote nayeye yupo tayari kupambana nae kwani yeye anafuata sheria bali hafanyi kazi ya kuropoka kwenye vyombo vya habari.

No comments:

Post a Comment