HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, December 31, 2012

TANZIA- MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero afariki dunia


Na Senior Libonge,Kilombero

MWENYEKITI wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero Ramadhani Kiombile amefariki katika hospitali ya taifa ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Taarifa ambazo zimethibitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero Jackson Mpankuli zimesema kwamba Kiombile amefariki jana (leo) saa 6 mchana katika hospitali ya Taifa Muhimbili.

Mpankuli alisema Mwenyekiti huyo alikuwa anaumwa huku akikataa kueleza ugongwa uliokuwa ukimsumbua na kwamba sababu zilizopelekea  kifo chake zitaelezwa baadaye baada ya madaktari wa hospitali hiyo kuufanyia uchunguzi mwili huo.

Mkurugenzi huyo alisema kwa upande wa suala la maziko bado ni mapema kulizungumzia na kwamba watalitolea ufumbuzi baada ya kumalizika kwa kikao cha pamoja kati ya viongozi wa serikali na halmashauro.

Taarifa za kifo cha mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero kimestua wakazi wengi wa wilaya hiyo ambao wengi wao wamekaa katika makundi makundi na wakijadili baada ya kupata taarifa hiyo huku wengi wao wakiwa hawaamini.

Baada ya kupata taarifa za msiba huo kila mwananchi wa wilaya ya Kilombero amekuwa akimpigia simu mwenzie ili kupata ukweli wa kifo hicho na baada ya kupatwa ukweli kila mmoja amekuwa na majonzi hasa kutokana na uwajibikaji wa mwenyekiti huyo kijana.

 

Marehemu Kiombile licha ya kuwa mwenyekiti  wa kwanza mdogo kuongoza halmashauri hiyo pia alikuwa diwani wa kata ya Ifakara kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM).

Atakumbukwa kwa mengi hasa ushirikiano kati yake na vijana katika kata yake na wilaya yote kiujumla pia msimamo wake ambapo alikuwa ahofii kumwambia mtu ukweli pale anapopata taarifa fulani ambayo inataka kurudisha nyumba maendeleo ya wilaya ya Kilombero.

Pia Kiombile anaheshimiwa baada ya kusimamia utengenezaji wa barabara za mitaa ya kata nzima ya Ifakara ambayo kwa hivi sasa zinapitika kwa msimu mzima na pia zinarahisisha mgeni yeyote anaeingia katika mji mdogo wa Ifakara kufika popote atakapo punde atakapoulizia.

Licha ya hayo pia marehemu alikuwa akisaidia watu wa aina mbalimbali wanaofika katika ofisi yake wakihitaji msaada wa fedha kwa ajili ya matibabu,shule na shida mbalimbali ambapo yeye alitoa fedha zake mfukoni na kuweza kuwasaidia.

Wakizungumza na gazeti hili wakazi wa mji wa Ifakara wamesema kuwa wilaya imempoteza kijana mchapakazi ambaye uwezo wake ulikuwa unahitajika zaidi hasa baada ya kufanya mambo makubwa punde alipopata vyeo hivyo vya uwenyekiti na udiwani.

Hiyari Bohari mkazi wa Ifakara amesema yeye baada ya kupata taarifa ilibidi akae kimya na kutoamini hasa kutokana na ukaribu alionao kati yake na mwenyekiti huyo hata kabla hajawa diwani na nafasi ya uwenyekiti.

 

“Unajuwa huwezi amini unapopata taarifa za ghafla kama hizi hasa kutokana na ukaribu wa mtu mwenyewe kwani marehemu nilikuwa nae karibu sana wakati tukiwa pamoja katika shughuli za usambazaji wa pembejeo na yeye kusema kuwa anaamua kuingia katika siasa na kweli dhamira yake ilifanikiwa kwa kupata udiwani na uwenyekiti,”alisema Hiyari.

Naye John Torogo mkazi wa Kidatu wilayani hapa alisema kuwa kifo cha Kiombile ni pigo kwa vijana wote wa wilaya hiyo kwani alikuwa mpiganaji wa kweli bila kuhofia mtu wala chama kwani alikuwa akisimamia haki katika kutatua matatizo mbalimbali ya wananchi katika wilaya ya Kilombero.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo David Ligazio alisema kuwa aamini mwenyekiti wake amefariki dunia kwani mara kwa mara alikuwa akiwasiliana na mtu wa karibu aliyekuwa akimuhudumia na kumuelezea kuwa afya yake inaimarika ila alipopigiwa simu na kaimu mkurugenzi pamoja na mkuu wa wilaya nguvu zote zilimuishia.

Naye mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilombero Abdallah Kambangwa amesema kuwa naye ameshtushwa na habari za msiba huo kwani marehemu alikuwa akishirikiana nae vizuri ndani ya kazi za chama na za nje ya chama akimchukulia kuwa ni mdogo wake hivyo asingekubali apotosheke wakati yeye yupo

 

No comments:

Post a Comment