HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Saturday, December 15, 2012

Tulinde Misitu yetu na rasilimali adhimu, wananchi waaswa


Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero.

Serikali imeahidi kwa dhati kabisa kusimamia Sheria za Uhifadhi wa Misitu .

Akifunga Warsha ya Siku Moja ya Uwasilishaji wa Hali Halisi ya Hifadhi ya Misitu ya Udzungwa, Bi Hawa Mposi Lumuli, Afisa Tarafa ya Ifakara amesema kwa Watumishi wa Idara ya Misitu wanaolegalega na kutosimamia ipasavyo Sheria, Kanuni na Taratibu na kukiuka maadili watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Amesema kuwa tegemeo kubwa la Serikali ni kuona wafanyakazi wa Idara hiyo wanazingatia maadili na kusaidia kuokoa, kuhifadhi na kutunza misitu.

Kwa upande wao watafiti kutoka Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania(TFCG) wamesema kuwa Hifadhi ya Milima ya Udzungwa imeonekana ya Kipekee kwa Uhifadhi wa Wanyama muhimu na Adimu kama Swala waitwao Vinde na Vyura wa Kihansi.

Vinde, aina ya Swala adimu Misitu ya Asili ya Udzungwa.

Akiwasilisha Matokeo ya Utafiti wa Hali ya Msitu wa Udzungwa, Bwana Justine Gwegine ,Afisa Mtafiti  na Mtathimini wa Hali ya Misitu kutoka Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania(TFCG) amesema kuwa  Matokeo ya  ya utafiti wao yameorodhesha Jumla  ya aina za ndege 79 zilionekana na katika maeneo  ya Ikule, Chita Wilayani Kilombero na Illutila na Idegenda katika Wilaya ya Kilolo.

Amesema kuwa kati ya  aina 79  zilizoorodheshwa, aina 14  ambayo  ni asilimia 17 ni wale ndege adimu na pengine wanapatikana katika  tao la  mashariki pekee.


Mbega mweupe, kiumbe adimu anyepatikana katika msitu wa Udzungwa
Lengo la Uwasilishaji huo ni kufahamu hali ya Misitu na Bioanuai yake kwa ujumla ili kuisaidia Serikali Kupanga Mipango ya Kuisimamia Vizuri kutokana na Matokeo ya Tafiti.

Utafiti huo umefanyika kwa Siku 25 Mwezi Septemba na Oktoba mwaka jana ambapo Vijiji Vinne vya Wilaya za Kilolo na Kilombero zimehusika.







Msitu wa Hifadhi Asili wa Udzungwa wenye ukubwa wa Hekta  20,720 na ulianzishwa Mwaka 1929, unasimamiwa na Wakala wa Misitu Tanzania.



No comments:

Post a Comment