HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, December 11, 2012

Mkuu wa Wilaya apania kuweka safi mji wa Ifakara


Na Igamba Libonge,Kilombero

KATIKA kuonyesha kukerwa na uchafu uliokithiri katika vizimba vya madampo madogo matatu yaliyopo katikati ya mamlaka ya mji mdogo wa Ifakara,mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala ametoa masaa 24 kwa viongozi wa mamlaka huo kuondoa uchafu huo la sivyo wahusika wote watawajibishwa kisheria.

Masala ametoa agizo hilo jana wakati alipotembelea na kujionea lundo kubwa la takataka zikiwa zimelundikana katika vizimba hivyo hivyo vitatu ambavyo ni vya stendi ya mabasi,stendi ya zamani na soko kuu la Ifakara.

Katika ziara hiyo sehemu ya kwanza kutembelea ilikuwa stendi ya mabasi ambapo wananchi walimweleza mkuu huyo wa wilaya kuwa licha ya wao kuchangia lakini wanashangaa taka hizo kuendelea kujaa na wanaosababisha kujaa huko ni majirani ambao utoa taka zao majumbani na kuzileta katika dampo hilo.

Sehemu ya pili kutembelea ilikuwa stendi ya zamani ambapo hapo alikuta takataka zimelundikana hadi barabarani na wakazi wa maeneo hayo walimweleza mkuu huyo kuwa wanashindwa kukaa katika maeneo yao hasa kutokana na harufu kali inayotoka katika dampo hilo.

Alipofika sokoni ndipo alipopata malalamiko mengi kutoka kwa wafanyabiashara wa soko hilo ambapo wamedai kuwa licha ya kulipia ushuru kwa kila siku wanashangaa takataka hizo kuendelea kuwepo eneo hilo na malalamiko yao pamoja na kukosekana kw walinzi wenye silaha na geti walikwisha ueleza uongozi wa halmashauri kwa muda mrefu lakini hakuna mabadiliko.

Kauli hiyo iliungwa mkono na mwenyekiti wa wafanyabiashara wa soko hilo Shabani Gwazai ambaye alisema kuwa licha ya kukutana mara kadhaa na uongozi wa halmashauri kuhusu kutatua matatizo hayo hakuna jipya lililojitokeza na kusema kuwa kama ukiwepo ushirikiano wa pamoja kati ya wao kama wafanyabiashara na halmashauri tatizo la uchafu halitakuwepo sokoni hapo.

Awali kabla ya kutoa fursa ya maswali kwa wafanyabiashara taarifa ya afya ya kata ilisomwa na kueleza changamoto wanazokabiliana nazo ikiwemo kutokuwa na vyombo vya usafirishaji taka vya uhakika,matumizi mabaya ya vizimba ikiwemo jamii kutupa vinyesi na mimba zilizotolewa mitaani na jamii kutumia watu wenye mtindio wa ubongo kutupa taka kwenye vizimba.

Changamoto nyinngine ni mwitikio mdogo wa jamii juu ya usafi wa mazingira na baadhi ya wanajamii kukaidi uondoaji wa takataka kwenye misingi ya barabara kwa madai kuwa shughuli hiyo ni ya halmashauri hata hivyo wamesema matumizi ya sheria ndogo za mamlaka ya mji mdogo itakuwa ufumbuzi mkubwa na suluhisho la tatizo hilo sugu.


Ndipo ilipofika zamu ya mkuu wa wilaya kuongeza na kutoa masaa 24 kwa taka zote zilizopo katika vizimba hivyo vitatu kuzolewa haraka na kama akiendelea kuziona wahusika wote watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Masala amesema ameaumua kufanya ziara ya kutembelea vizimba hivyo baada ya kupata malalamiko ya kukithiri kwa uchafu ukizingatia kuwa vizimba hivyo vipo katikati ya mji wa Ifakara ambao ndio kioo cha wilaya ya Kilombero kwani alikwisha toa agizo kwa watendaji wa mji huo wahakikishe kuwa uchafu usiwepo tena katika vizimba hivyo.

Amesema kuwa aimuingii akilini kuwa uchafu huo unaendelea kulundikana katika vizimba hivyo wakati wananchi na wafanyabiashara wanalipa ushuru hivyo kuutaka uongozi wa kata kubuni njia nyingine itakayosaidia kupunguza taka katika vizimba hivyo ikiwemo kuweka sheria za utupaji wa taka.

Hata hivyo Masala amemtaka mtendaji wa kata ya Ifakara kumkamata kisha kumfikisha kwenye vyombo vya sheria mtu yeyote atakaebainika kuwa anatupa taka nje ya vizimba vilivyowekwa na halmashauri.

Kwa upande wake bwana afya wa wilaya Mbonja Kasemba alisema kuwa katika bajeti ya mwaka huu idara ya afya imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika dampo kubwa la Kiogosi ili kuzuia wananchi kuzitoa taka punde zinapomwagwa na pia wanategemea kujenga kibanda kwa ajili ya walinzi eneo hilohilo la Dampo.

No comments:

Post a Comment