HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Saturday, December 1, 2012

Gharama za Afya zapanda katika Hospitali ya St. Francis Ifakara


Na Senior Libonge,Kilombero

KUTOPATA fedha kwa wakati kutoka mfuko wa pamoja(basket fund)na mgawanyo mdogo toka bohari ya madawa nchini(MSD)ndiko kunakosababisha hospitali ya rufaa ya Mt.Francis iliyopo mjini Ifakara wilayani Kilombero kupandisha gharama ya matibabu.

Akizungumza katika kikao cha kamati ya ushauri ya wilaya,mkurugenzi wa hospitali hiyo Dk,Angelo Nyamtema amesema licha ya kutopata fedha kwa wakati na mgawanyo mdogo pia suala la ulipaji wa mishahara kwa wataalamu mbalimbali nayo uchangia hospitali hiyo kukosa fedha.
                
Dk,Nyamtema amesema licha ya changamoto hizo alizozitaja mkakati uliopo hivi sasa ni kuboresha huduma katika hospitali hiyo ili kuweza kufikia hadhi ya hospitali ya rufaa baada ya kupandishwa hadhi.

Amesema ni mwezi wa tano hivi sasa hawajapata fedha ya basket fund huku pia wakiwa hawajapata fedha toka serikalini tokea mwezi Julai mwaka huu ili kuweza kuagiza madawa na vifaa mbalimbali vya tiba kutoka bohari ya madawa nchini(MSD).

Mkurugenzi huyo wa hospitali ameiomba halmashauri ya wilaya na serikali kiujumla kushirikiana nao ili kutatua changamoto zinazowakabili hatimaye kuweza kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi wanaotumia hospitali hiyo kutoka sehemu mbalimbali nchini.

Amesema suala la mishahara limekuwa tatizo kwani kwa kipindi cha karibuni wametumia kiasi cha shilingi milioni 42 kwa ajili ya kulipa mishahara watumishi wake na fedha hizo zimetokana na fedha zinazotokana na gharama za uchangiaji zinazotozwa kwa wagonjwa.

Dk,Nyamtema ameiomba serikali kuwapatia wataalamu walioajiriwa na serikali ili wao waweze kupunguza mzigo mkubwa wa kuwalipa mishahara na hali hiyo itapelekea kupunguza gharama kwa wananchi wanaopata huduma katika hospitali hiyo.

Hata hivyo mkurugenzi huyo amekanusha taarifa kuwa menejimenti ya hospitali uamua kupandisha gharama za matibabu wanapojisikia na kusema kuwa mawazo ya kupandisha gharama za matibabu sio ufanywa na uongozi wa hospitali bali ni kamati nzima inayowashirikisha watu kutoka serikalini,halmashauri ya wilaya na wadau mbalimbali.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kilombero aliuagiza uongozi wa halmashauri ya wilaya chini ya mwenyekiti wake na mkurugenzi mtendaji kukaa pamoja na menejimenti ya hospitali hiyo ili kutatua matatizo mbalimbali hatimaye kuweza kumpunguzia mwananchi mzigo wa gharama za matibabu.


No comments:

Post a Comment