HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, November 27, 2012

SUALA LA ARDHI BADO LAFUKUTA KILOMBERO


Na Senior Libonge,Kilombero

SERIKALI wilayani Kilombero imesema kuwa itafuta mpaka wa kugawa ardhi ya kijiji na hifadhi bila kujali gharama iliyotumika kama ikibainika kuwa mpaka huo umekosema.

Kauli hiyo imetolewa jana na mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji cha Miwangani kata ya Idete baada ya wananchi hao kulalamika mbele ya mkuu huyo wa wilaya kuwa mpaka uliowekwa hivi karibuni kutenganisha kijiji na eneo la hifadhi umemega sehemu kubwa ya ardhi ya kijiji.

Hivi karibuni halmashauri ya wilaya ya Kilombero iliweka mpaka wa kutenganisha vijiji na eneo la hifadhi la lengo ni kuyatenganisha maeneo hayo ni kutekeleza azimio la Ramsar lililotaka kutunza maeneo ya ardhi oevu ambayo yana umuhimu wa pekee duniani katika suala zima la utunzaji wa mazingira.

Hata hivyo zoezi hilo lililofanywa na wataalamu wa mazingira na ardhi wa wilaya lililalamikiwa na baadhi ya wananchi ambapo mpaka huo umepita kuwa wataalamu hao walikuwa wakifanya kazi bila kushirikisha serikali za vijiji ambazo zinajuwa mipaka halisi ya vijiji vyao na eneo la hifadhi.

Masala amesema kuwa ameamua kufika katika kijiji hicho ili kupata ukweli kuhusu tatizo la mipaka baada ya kupata barua na kupigiwa simu kutoka kwa viongozi wa kijiji na wananchi kuwa wataalamu walikwenda kuweka mpaka wamemega sehemu kubwa ya kijiji na kufanya wananchi wa kijiji hicho kukosa ardhi kwa ajili ya shughuli za kilimo na mifugo.

Na alipotoa nafasi kwa wananchi ili kutoa kero zao wananchi wote waliosimama walilalamikia suala la mpaka na kusema kuwa kama serikali isipochukua hatua za haraka kurekebisha mpaka huo kuna hatari ya kutokea kwa mapigano kati ya wakulima na wafugaji kwani hivi sasa mifugo iliyopo katika kijiji hicho inalishiwa katika mashamba ya wakulima kwa kukosa sehemu za malisho ambazo mwanzo zilitengwa eneo lililomegwa.

Ilibidi mkuu wa wilaya aingilie kati kupunguza hasira baada ya kutokea hali ya kutupiana maneno makali waliokuwa wakirushiana kati ya wataalamu wa ardhi na maliasili na mwenyekiti wa kijiji cha Miwangani Abdul Mtilangondo ambapo kila mmoja alikuwa akijitetea kuwa yupo sawa katika suala hilo.

Baada ya wataalamu kusema kuwa mpaka uliowekwa ni halali kwani wametumia kifaa maalum cha kupimia GPS na wakati wanaendesha zoezi hilo walishirikisha serikali ya kijiji lakini wakati zoezi linaendelea mwenyekiti wa kijiji aliwashawishi wajumbe wa serikali ya kijiji kususia zoezi hilo.

Naye mwenyekiti wa kijiji Mtilangondo alisema kuwa wakati zoezi linafanyika aliamua kugoma kutokana na wataalamu hao kupindisha mipaka wakati ramani halali inaonyesha mipaka inapotakiwa kupita lakini wataalamu hao wanagoma na kuweka mipaka wanayotaka wao na hali hiyo ndiyo ilipelekea yeye na wajumbe wake kususia zoezi hilo.

Ndipo mkuu wa wilaya alipoamua kuingilia kati na kusema kuwa itabidi zoezi hilo liangaliwe upya kati ya wataalamu wa halmashauri na viongozi wa serikali ya kijiji na ikibainika kuwa mipaka imekosewa itafutwa na kuwekwa upya bila kujali gharama iliyotumika ila ikionekana na halali itabidi mipaka hiyo iheshimiwe.

Masala alisema cha msingi ni kulinganisha mipaka halali kwa kufuata ramami za vijiji husika na ramani za wilaya kwani zoezi hilo sio la kuwakomoa wananchi bali ni kuyahifadhi maeneo ambayo kwa kiasi kikubwa yameharibika baada ya kuvamiwa na kusema kuwa kama mipaka ipo halali yeye hana mamlaka ya ubadilishaji wa mpaka huo.

No comments:

Post a Comment