HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, November 12, 2012

Operesheni Okoa Bonde Tengefu la Kilombero yakabiliwa na changamoto


Henry Bernard Mwakifuna, Mchombe-Kilombero

KUTOKUWAPO kwa utaratibu mzuri unaotumika kuwasimamia ili kuhakikisha Wafugaji Wavamizi wanatoka nje ya Wilaya ya Kilombero imekuwa Changamoto mojawapo katika Operesheni Okoa Bonde la Kilombero.

Bwana Madaraka Amani, AfIsa Wanyamapori Wilaya ya Kilombero amewambia waandishi wa Habari waliotembelea operesheni hiyo kuwa wavamizi wanaotozwa faini na kuamriwa kuondoka nje ya Wilaya hii wamekuwa wanazunguka zunguka ndani ya Wilaya hiyo na kisha kurudi kufuatia kutokuwapo Utaratibu mzuri.

Amesema kuna tetezi za suala hilo na Watakaobainika watapelekwa moja kwa moja Mahakamani kwani watakuwa wamevunja Sheria na kukiuka maagizo ya Serikali.

Ameongeza kuwa Wafugaji Wavamizi awali waliekezwa waende Lindi  ambapo walitengewa maeneo na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bwana Said Mecky Sadiq kwa zaidi ya Ng’ombe Laki moja ambapo Takwimu zinaonesha ni N’gombe Elfu Ishirini na mbili tu ndiyo walioenda huko.

Sababu kubwa anabainisha Bwana Madaraka ni kuwa Bonde la Kilombero lina malisho bora yenye Virutubisho kwa Mifugo inayopelekea Mifugo kama N’gombe kuzaa kila Mwaka hivyo kupelekea Wafugaji kukahidi kuondoka.

Wakati huo huo, Bwana Madaraka Amani amesema kuwa Sheria Tisa zinatumika katika operesheni okoa Bonde Tengefu la Kilombero.

Amezitaji Sheria hizo kuwa ni  Sheria ya Mazingira, Sheria ya Wanyamapori, Sheria ya Misitu na Sheria ya Ardhi ya Vijiji.
Nyingine ni Sheria ya Uhamishaji wa Mifugo, Sheria ya Kuweka Alama Mifugo na Sheria ya Mipango ya Matumizi bora ya Ardhi.

Operesheni Okoa Bonde Tengefu la Kilombero lenye Ukubwa wa Kilometa 7,697 likihusisha Vijiji 228 limeanza Tangu Mwishoni mwa Mwezi Uliopita na katika Wilaya ya Kilombero ilianzia katika Tarafa ya Mlimba na kwa sasa ipo Kata ya Mchombe.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Bwana Elias Masala amesema kuwa Sheria kuu zinazotumika katika Operesheni hii ni ile ya Wanyamapori kipengele cha 116 (2) kisemacho Afisa amepewa kutoza faini ya kiwango kisichopungua Elfu 20 na kisichozidi shilingi Milioni 10 kwa kosa moja.

Sheria ndogondogo za Kilimo na Mifugo chini ya Halmashauri za mwaka 2007 sheria kifungu cha 10 kinachosema faini isizidi shilingi Laki Tatu ni sheria ya pili inayotumika katika operesheni Okoa Bonde la Kilombero.

Kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero kwa sasa wanatoza Faini ya Kati ya Shilingi Elfu 10 na Elfu 40 kwa kosa moja.

No comments:

Post a Comment