HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Saturday, November 3, 2012

Hali ya upatikanaji wa Mafuta yawa shwari Kilombero


Na Senior Libonge,Kilombero

HALI ya upatikanaji wa nishati ya mafuta katika wilaya ya Kilombero imerudi kama kawaida kwa bidhaa hiyo kuanza kupatikana baada ya kuadimika kwa wiki moja sasa.

Kukosekana kwa nishati hiyo muhimu ikiwemo Petrol,Diseli na mafuta ya taa kulisababisha walanguzi kupandisha bei ya mafuta kwa bei wanayotaka wao na ilipelekea bei ya petrol kufikia shilingi 5000 badala ya bei halisi ya shilingi 2360.

Bei ya petrol ilikuwa juu zaidi hasa baada ya kutumiwa na wananchi wengi hasa waendesha pikipiki maarufu Bodaboda ambapo na wao ilipelekea kupandisha nauli ya safari kutoka shilingi 1000 hadi kufikia shilingi 2000.

Licha ya kupanda kwa bei huko na bidhaa hizo kuuzwa kwa kificho jeshi la polisi liliendelea na msako wa kuwakamata walanguzi hao ambao wengi wao walificha bidhaa hiyo kwenye nyumba zao bila kuhofia hatari ya kulipuka na kusababisha moto katika nyumba hizo.

Kutokana na tatizo hilo wengi wa wananchi wilayani hapo waliwalaumu wamiliki wa vituo vya mafuta kuwa walikuwa wanakataa kwa makusudi kuyatoa mafuta ambayo yalikuwemo kwenye matanki yao kwa kutaka yapandishwe bei na wao wayatoe huku wengine wakisema kuwa pia wamiliki hao walikuwa wakiwatumia walanguzi kwa kuwapa mafuta nyakati za usiku ili asubuhi wayauze kwa bei ya juu.

Kwa upande wao wamiliki wa vituo vya mafuta wote kwa pamoja baada ya kuhojiwa walisema kuwa kukosekana kwa bidhaa hiyo Dar es Salaam ndiko kulikofanya wao wakose nishati hiyo na pia kukanusha kuwa hawakuwa wakitoa mafuta kinyemela kwa ajili ya kuwapatia walanguzi ili wawauzie kwa bei ya juu.

Hata hivyo huduma hiyo imerudi katika hali ya kawaida tokea Novemba 3 ambapo mafuta yameanza kuuzwa katika vituo vya mafuta katika mji wa Ifakara na katika tarafa ya Kidatu huduma hiyo ilianza kupatikana tokea Novemba 1 mwaka huu.

Mwandishi wa habari hii alishuhudia misururu mirefu wa magari na pikipiki katika moja ya kituo cha mafuta Ifakara na wengi wao walisema kuwa licha ya kujaza matenki ya vyombo vyao vya moto pia wataweka akiba kwani hawawaamini tena wamiliki wa vituo vya mafuta na kuhofia kuwa watawadanganya na kuwaeleza kuwa yamekwisha kumbe wamehifadhi kwenye matanki yao.

No comments:

Post a Comment