HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Wednesday, October 31, 2012

WAFUGAJI WAVAMIZI, WAKULIMA WALIOINGIA HIFADHINI KUONDOKA KWA NGUVU

Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero.

SERIKALI Wilayani Kilombero imetangaza kwa Wafugaji wavamizi walioshauriwa kuondoka waanze kufanya hivyo kabla ya Oparesheni maalumu ya kuwaondoa kuanza Rasmi Mwisho wa Mwezi Oktoba.

Bwana Hassan Masala,Mkuu wa Wilaya ya Kilombero katika Tangazo alilolitoa amesema kuwa wale wote Wafugaji wenye mifugo mingi waliovamia maeneo yasiyoruhusiwa waondoke mapema kabla ya tarehe 30 Oktoba 2012 ambapo oparesheni maalum itaanza.
Ametanabaisha kuwa Wafugaji wavamizi ni wale walioingia kijijini bila ya kupokelewa na Serikali ya kijiji na Kuthibitishwa na Mkutano wa Kijiji huku pia kukiwa na kundi jingine la Wafugaji lenye Mifugo ambayo haijapigwa Chapa na kutambuliwa na Serikali kufuatana na eneo la Malisho lililotengwa kwa Kijiji husika.

Wataalamu wa Idara ya Mifugo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero wametenga maeneo ya Malisho kwa Kila Kijiji chenye Wafugaji huku eneo hilo likipimwa kwa idadi maalumu ya Mifugo inayotakiwa kuwepo kutokana na ukubwa wa eneo hilo.
Mbali ya Suala la Wafugaji wavamizi Mkuu wa Wilaya amewataka Wakulima waliovamia eneo la Hifadhi ambalo kisheria haliruhusiwi kufanyika shughuli za Kibinadamu  waondoke mara moja sanjari na Wafugaji wavamizi.

Serikali ilitangaza ifikapo Septemba 7 kuwa Mwisho wa kuondoa mifugo kwa Hiari Katika Bonde la Mto Kilombero lakini kutokana na shughulili za Kitaifa za Sensa na Mchakato wa kupata Katiba Mpya zoezi la kuwaondoa kwa nguvu likasogezwa mbele na kwa sasa limeandaliwa rasmi kuanza mmwisho wa Mwezi huu.

No comments:

Post a Comment