HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Wednesday, October 31, 2012

Madiwani upinzani wasusia kikao Kilombero


 Na Senior Libonge, Ulanga

MADIWANI wa kambi ya upinzani katika baraza la halmashauri ya wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro jana walilazimika kutoka nje na kususia kikao cha baraza hilo kufutia hoja ya kutaka diwani wa mteule wa viti maalum kupitia tiketi  ya chama cha wananchi (CUF),Maricena Mchanga, kutupiliwa mbali na baraza hilo.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa 5.00 asubuhi muda mfupi mara baada ya mwenyekiti wa baraza hilo, Furaha Lilonge, kufungua kikao hicho na kutaka madiwani kupitisha agenda za kikao hicho na baada ya hapo hoja ya kupishwa kwa diwani huyo ilijitokeza.

Kujitokeza kwa hoja hiyo pia kulifuatia mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Isabera Chilumba, kusema kuwa katika agenda za hikao hicho kulisahaulika agenda zingine mbili za kuapishwa kwa diwani huyo na kupokea ujumbe kutoka tume ya utumishi wa umma ambao ulitaka kuzungumza na baraza hilo.

Hoja ya mkurugenzi huyo ilizua mabishano baina ya madiwani wa halmashauri hiyo huku upande wa madiwani kutoka chama tawala chama cha mapinduzi (CCM), wakitaka kanuni za uendeshaji wa kikao cha baraza zizingatiwe kwa madai kuwa kuapishwa kwa diwani huyo kulipaswa kufanyika kabla ya kufunguliwa kwa kikao hicho na kwamba kikao hicho kwa vile kilikwisha anza hakikuwa sahihi kutumika kumuapisha.

Kauli hiyo aliyotolewa na diwani wa wa kata ya Mawasiliano katika tarafa ya Mahenge, Mwanaidi Mkalimoto, na kupingwa vikali na kambi ya upinzani ikiongozwa na diwani wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema), Said Tilla, ambaye alitaka haki ya diwani huyo mteule izingatiwe.

Hata hivyo, malumbano hayo yalimlazimu mwanasheria wa halmashauri hiyo, Bahati Kikoti, kutoa ufafanuzi kuwa kanuni za wizara ya tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI), kuhusu uapishwaji wa madiwani zinaeleza kuwa diwani ataapishwa kabla ya kikao chake cha kwanza na kushauri kuwa bado agenda ya kuapishwa kwa diweani huyo ingeingizwa katika agenda za kikao hicho.

Licha ya kutoa ufafanuzi huo wa mwanasheria, lakini mwenyekiti alisimamia hojas yake kwa kusema kuwa agenda ya kuapishwa kwa diwani huyo mteule haitaingizwa miongoni mwa agenda hizo kutokana na kanuni za uendeshaji wa baraza hilo kwa madai kuwa kwa kuwa madiwani walikwisha pitisha agenda hizo agenda za ziada hazitaruhusiwa.

Hatua hiyo ya mwenyekiti wa halmashauri iliwalazimu madiwani tisa wa kambi ya upinzani kunyanyuka na kutoka nje wakipinga kuondolewa kwa hoja hiyo.

Diwani wa kata ya Lupiro (Chadema), Nassoro Mcharange ameiambia blog hii kuwa maamuzi yaliyotolewa na mwenyekiti wa halmashauri hiyo hayakuwa sahihi kwa vile diwani mteule alifika katika baraza hilo kufutia barua ya halmashauri yenye kumbukumbu namba UDC/ADM/E.20/4/35 ikimtaka diwani huyo mteule kuhuzulia kikao hicho ili kuapishwa na kushiriki kikao.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Sofi katika tarafa ya Beatus Daud, kupitia tiketi ya TLP, alilalamikia maamuzi yanayotolewa na mwenyekiti huyo kwa mdai kuwa amekuwa akiegemea kwenye chama chake cha CCM.
Hata hivyo, mwenyekiti wa halmashauri hiyo akijibu tuhuma hizo alisema kuwa uendeshaji wa baraza hilo amekuwa akiufanya kwa kuzingatia kanuni za uendeshaji baraza tofauti na madai yanayotolewa na madiwani wa kambi ya upinzani.

Akitoa ufafanuzi wa madiwani hao kususia kikao hicho na kutoka nje alisema kuwa yako makosa yaliyofanywa na halmsahuri hiyo juu ya uteuzi wa diwani mteule huyo kwa maelezo huwa chama cha CUF kinadiwani mmoja wa kuchaguliwa hivyo hakikuwa na sifa ya kuwa na diwani wa viti maalum.

Alidai kuwa chama cha Chadema na TLP vimekuwa na sifa hiyo kutokana na kuwa na madiwani watatu kila kimoja na CCM ilipata madiwani wanane wa viti maalum kwa kuwa na madiwani 24 wa kuchaguliwa na wabunge wawili na kwamba kwa sifa ya diwani watatu kukiwezesha chama kupata diwani wa viti maalum basi sifa hiyo ilikuwa ni CCM kuongezewa diwani mmoja na siyo CUF.


“Tatizo linaonekena liko kwenye uongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo kwa kuipotosha tume ya uchaguzi kuipatia taarifa zilizoiwezesha tume kumteua diwani wa CUF, haki hiyo ilikuwa ni ya CCM hivyo CCM wanapaswa kuidai haki hiyo,” alisema Lilongeli.

Naye diwani mteule aliyetarajiwa kuapishwa katika baraza hilo, Mchwanga, alisema kuwa kutokjuapishwa kwake katika kikao hicho kumemsikitisha kwa vile aliandikiwa barua na halmsahuri kuhusu uteuzi uliofanywa na tume ya uchaguzi Agosti 14, mwaka huu na kumtaka kuhuzulia kikao hicho ili aweze kuanza kutekeleza majukumu yake.

No comments:

Post a Comment