HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Wednesday, October 31, 2012

WAASWA KUFUATA SHERIA KATIKA ZOEZI LA KUONDOA WAFUGAJI KILOMBERO


Na Henry Bernard Mwakifuna, Itete-Ulanga

WATUMISHI watakaohusika na Operesheni Okoa Bonde la Kilombero wametakiwa kutenda Haki kwa Kufuata Sheria.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwana Saidi Mecky Sadiq amesema kuwa suala la uonevu na ukihukwaji wa sheria halina nafasi katika  zoezi la kuwaondosha Wafugaji na Wakulima Wavamizi kuwa watakaobainika watachukulia Hatua kali dhidi yao kwa muujibu wa Sheria.

Amewataka Maaskari watakaoendesha Operesheni hiyo kutotumia Nguvu isiyo ya Lazima kupita kiasi huku akiwataka pia Wananchi nao kutochukua sheria mkononi kwa Silaha za jadi ili kuepusha mapambano baina yao.

Bwana Sadiq ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam alikuwa Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Operesheni Okoa Bonde la Kilombero iliyofanyika katika Kata ya Itete Wilayani Ulanga.

Wakati huo huo Mifugo itakayokamatwa ndani ya Hifadhi ya Pori Tengefu la Kilombero itapigwa Mnada kwa Muujibu wa Sheria.

Bwana Hassan Masala, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero akisoma Taarifa ya Hali Halisi ya Bonde la Kilombero amesema Mifugo hiyo pamoja na ile isiyosajiliwa na kupigwa Chapa itauzwa na Serikali kwa kufuata utaratibu wa Kisheria ulioandaliwa.

Amesema Vituo 11 vimetengwa  kwa Wilaya za Ulanga na Kilombero kwa ajili ya kuhifadhia Mifugo itakayokamatwa kwa kukihuka utaratibu.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Kilombero alikuwa akisoma Taarifa iliyoandaliwa juu ya Hali Halisi ya Bonde la Mto Kilombero linalojumiisha  Wilaya za Ulanga na Kilombero Mkoani Morogoro.

No comments:

Post a Comment