HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, October 23, 2012

Wafugaji Ulanga/Kilombero hatarini kukubwa na baa la njaa

Na Senior Libonge, Ulanga.

ZAIDI ya kaya 250 za wafugaji wa jamii ya wasukuma zipo katika hatari ya kukumbwa na janga la njaa baada ya familia hizo kudaiwa kuacha mazao ya chakula wakati wa operesheni ya kuwaondoka kwa hiyari wafugaji katika bonde la hifadhi la mto Kilombero kwa upande wa wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro.

Akizungumza na Blog hii katika kijiji cha Kiwale kitongoji cha Lubemende tarafa ya Malinyi Mwenyekiti wa Umoja wa wafugaji wilaya hiyo (UWADAMO), Luhende Maduka Ng’asha alisema kuwa zaidi ya kaya 250 za wafugaji wa jamii ya wafugaji zipo katika hatari kubwa ya kukumbwa na baa la nja baada ya wafugaji hao kuacha mazao ya chakula katika operesheni iliyoanza Septemba 8 mwaka huu.

Ng’asha alisema kuwa baa hilo la njaa linaweza kujitokeza endapo serikali haitafanya juhudi za haraka za kuzinusuru familia hizo kwa kuzipatia maeneo ya kulima mazao ya chakula ikiwemo na malisho kutokana na baadhi ya familia hizo kuwa na akiba kidogo ya chakula kufuatia chakula cha ziada kutelekezwa mashambani kabla ya kufunwa wakati wa operesheni hiyo.

Vyakula ambavyo vinadaiwa kutekezwa ndani ya hifadhi hiyo kabla ya kuvunwa ni pamoja na mpunga, mihogo na viazi ambavyo vilikuwa katika hatua za mwisho ya kuvunwa kwake.

Ng’asha alisema kuwa familia za wafugaji hao zinahitaji kupatiwa msaada wa haraka hasa baada ya kukosa maeneo ya kulima na maeneo ya malisho kufuatia maeneo ambayo walikuwa wakiishi kuingizwa ndani ya hifadhi ya bonde hilo la mto Kilombero.

Hatua hiyo ya familia hizo kuacha mazao ya chakula katika maeneo yao ambayo walikuwa wakiishi kwa muda mrefu imekuja baada ya awamu ya pili ya uwekaji wa alama za mipaka kutengenisha hifadhi na vijiji hali ambayo awamu hiyo ya pili imeweka njia panda kufuatia kuingia ndani ya hifadhi huku baadhi ya vijiji vikidaiwa kubakiwa na maeneo madogo ya ardhi kwa ajili ya matumizi ya mpango wa matumizi bora ya ardhi. Alisema Ng’asha.

Ng’asha alisema kuwa kwa sasa familia hizo zimekuwa zikiishi katika mazingira magumu zaidi kutokana na kuacha makazi yao ya kudumu zikiwemo nyumba na mashamba ambayo yalikuwa yakitumiwa kwa ajili ya kilimo na nyumba za kudumu baada ya alama za mipaka ya awamu ya pili.

“Hapa kuna janga la njaa litatokea muda wowote kwa familia za wafugaji ambao wengi wao ni wale ambao walikuwa wakiishi nje ya hifadhi ya bonde la mto Kilombero lakini hali hiyo imetokana na mipaka ya awali kuwakuta wapo nje ya hifadhi na awamu ya pili mipaka hiyo imewakuta wapo ndani ya hifadhi hivyo na kuleta hali ya taharuki kwa familia hizo. Alisema Ng’asha.

Aliongeza kuwa familia hizo baada ya kuacha mazao ya chakula katika maeneo hayo imejikuta ikibakiwa na chakula kidogo ambazo hakikidhi mahijita kwani familia moja ina watu zaidi ya 30 na janga hilo la njaa linaweza kuwakumba kati ya Novemba na Disemba mwaka.

Wengi wao  kupoteza mwelekeo wa maisha ya baada ya wenzao ambao walielekea wilaya ya Namtumbo mkoani Songea kurudishwa katika wilaya ya Ulanga.

Operesheni ya wafugaji ya kuondoka katika bonde la Kilombero kwa hiyari  limewaweka njia panda wafugaji ambao walikuwa nje ya hifadhi hiyo ambapo kwa sasa shughuli za kilimo na malisho zimekuwa za shida kutokana na kuondoka ndani ya hifadhi na kuvamia maeneo mengine ambayo yaliyomilikishwa kihalali na wafugaji wengine.” alisema Ng’asha.

Ng’asha alisema kuwa katika mchakato wa kuelekea katika operesheni hiyo mambo mengi ya msingi hayakufuatwa na kukiuka baadhi ya taratibu za kisheria zilizowekwa na serikali ya Ulanga kwa madai kuwa baadhi ya watendaji wake waliwatoza wafugaji pesa nyingi isivyo halali.

Katika zoezi hilo la upigaji wa chapa mifugo ndilo moja ya mazoezi ambayo yanadaiwa kukiukwa kwa taratibu hasa baada ya watendaji hao kudaiwa kutoza kiasi cha pesa kuanzia sh 3,000, 5,000 na sh 10,000 kwa ng’ombe mmoja tofauti na kiasi cha sh1,000 ambacho kilitangazwa na wilaya hiyo.

“Hawa wafugaji ni moja ya jamii ambayo zimekuwa ikiishi kwa maisha duni hapa nchini na na kuonewa kutokana na ufahamu finyu hii imetokana na baadhi ya watendaji serikalini kutumia mwanya huo kujipatia pesa kwa kisingizio cha kukiuka baadhi ya sheria kwa wafugaji hao” alisema Mwenyekiti huyo.

Alitaja kero ambazo kwa sasa wafugaji hao wanazipata baada ya operesheni hiyo ni akinamama kujifungua chini ya miti, kukosa makazi na maeneo kwa ajili ya kilimo na malisho ambapo wafugaji hao waliingia katika maeneo hayo na kuishi zaidi ya miaka 20 kabla ya mwaka huu kutimuliwa kulingana na mipaka iliyowekwa.

Serikali ndiyo iliyotoa amri ya kuondoa wafugaji katika hifadhi ya bonde la mto Kilombero lakini pia inayo jukumu la kuwatafutia wafugaji maeneo ya malisho na pakuwa wafugaji wa jamii ya wafugaji wanajishughulisha na kufuga na kulima serikali nayo iliione hilo kwa kuwatafuatia maeneo kulingana na mahitaji yao. Ng’asha.

Mkuu wa wilaya ya Ulanga Francis Miti akizngumzia suala hilo alisema kuwa suala la njaa halitajitokeza kwa sababu ni kweli baadhi ya wafugaji waliacha vyakula katika maeneo hayo lakini serikali iliweka utaratibu mzuri wa wafugaji hao kuomba vibali na kumalizia kuchukua mazao hayo.

1 comment:

  1. wananchi watahadharishwe juu ya uuzaji wa mazao, japo mkuu wa wilaya ameondoa shaka la kujitokeza kwa suala hilo....

    ReplyDelete