HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, September 18, 2012

Ujenzi wa Daraja la Mto Kilombero kuanza rasmi


Na Senior Libonge,Ulanga

Serikali inakusudia kuanza ujenzi wa daraja la mto Kilombero ambalo linaunganisha wilaya za Kilombero na Ulanga katika Mkoa wa Morogoro  katika kipindi cha  mwaka huu wa fedha wa  2012/2013 

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejiment ya utumishi wa Umma  Celina Kombani, alitangaza kuanza kwa ujenzi huo  wakati akizungumza na wananchi wa kata za Ketaketa,Mwaya,Ilonga na Ruaha zilizopo katika jimbo la Ulanga mashariki mkoani Morogoro.

Alisema  kuwa tayari Serikali imeshapata fedha za kuanza ujenzi huo kinachofanyika hivi sasa ni kumpata mkandarasi ambaye atakamilisha ujenzi wake unatarajia kuanza katika kipindi hiki cha mwaka wa fedha .

Waziri huyo alisema kuwa tayari  Serikali ilishafanya upembuzi yakinifu katika mto kilombero kwa kutumia kampuni moja kutoka nchini Kenya ambayo ilitumia zaidi ya shilingi bilioni moja katika kazi hiyo.

Kutokana na hali hiyo Waziri  Kombani aliwataka wakulima kuanza kuzalisha mazao kwa tija na kuweza kuyaweka sokoni ili kukabiliana na ushindani kipindi daraja hilo litakapokamilika.

Katika hatua nyingine huo huo Waziri  Kombani amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuacha kuuza chakula walichokipata katika msimu wa kilimo uliopita ili kiweze kuwasaidia katika kipindi cha msimu wa masika ambao mara kadhaa wamekuwa wakikabiliwa na upungufu wa chakula.

Alisema katika kipindi hiki ni vema wananchi wakaelewa kuwa ni kipindi cha kujiwekea akiba ya chakula ili ije iwasaidie katika kipindi cha masika

1 comment:

  1. Ni hatua nzuri. Binafsi naona italeta mianya ya maendeleo kwa wilaya yetu. Kwa maana rahisi itapanua wigo wa biashara kwa wilaya za ulanga na kilombero...

    ReplyDelete