HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, September 10, 2012

MTENDAJI MACHIPI- IFAKARA MBARONI KWA UBADHIRIFU


Shule ya Sekondari Ifakara (Machipi), ikionekana kwa mbali




















Na Henry Bernard Mwakifuna, IFAKARA

Bwana  Ally Mahachi, Afisa Mtendaji wa kijiji cha Machipi Kata ya Michenga Wilayani Kilombero  anashikiliwa na  Jeshi la Polisi Wilayani humo kwa tuhuma   ya wizi wa fedha za Wananchi Shilingi Milioni Saba na Elfu Arobaini(7,040,000). 

Mtendaji huyo anashikiliwa na jeshi hilo tangu sept 4mwaka huu baada ya wananchi kuunda tume ya uchunguzi wa fedha za miradi iliyopo na inayotarajiwa kuanza na kugundua baadhi ya miradi mtendaji amewadanganya Wajumbe fedha zilizolipwa.

Baadhi ya wajumbe wa Serikali ya kijiji hicho wameeleza kuwa  kuna  Fedha zilitolewa na Mfuko wa Jimbo la Kilombero  kwa ajili ya Uchimbaji wa Visima vya Maji na uuzwaji wa eneo la ujenzi wa  Mnara tangu mwaka 2011, hata hivyo hadi sasa fedha hizo hazijulikani zilipo.



Njia ya kuelekea Mnarani

Wajumbe hao wamesema kuwa  Bwana Mhachi alifanya udanganyifu alipokuwa anatoa taarifa katika kijiji hicho cha Machipi kuwa amepokea shilingi laki saba(700,000) kwa ajili ya eneo la mnara hali ambayo siyo kweli. Uchunguzi wa Tume hiyo umegundua kuwa fedha zilizolipwa ni shilingi milioni 5,290,000/=na fedha zilizotolewa na mfuko wa jimbo ni shilingi milioni 1,750,000/= Jeshi la Polisi limethibitisha kukamatwa kwa Mtendaji huyo Bwana Mahachi akituhumiwa kula fedha za wananchi na upelelezi utakapo kamilika atafakishwa Mahakamani

Sehemu iliyouzwa kwa ajili ya ujenzi wa Mnara


No comments:

Post a Comment