HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, September 13, 2012

Wanakijiji Ruaha waangua Kilio mbele ya Waziri

Na Senior Libonge,Ulanga

KATIKA kuonyesha kuwa amekerwa na uharibifu mkubwa wa mazingira kwa ukataji na uchomaji ovyo misitu ya asili mwananchi wa kijji cha kituti tarafa ya Ruaha wilayani Ulanga,Metrucy Albert,ameangua kilio  mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Menejamenti ya Utumishi wa Umma,Celina Kombani wakati akimuelezea kukithiri kwa vitendo hivyo katika kijiji chao .
Albert aliangua kilio hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho baada ya kumalizika kwa hotuba  Waziri Kombani ambaye ni mbunge wa jimbo la Ulanga mashariki (CCM) baadaye na kuruhusu wananchi wa kijiji hicho kutoa kero zao mbalimbali zinazowakabili .
Baada ya kupewa nafasi hiyo kutoa kero hiyo,Albert alieleza kuwa hivi sasa kijiji hicho kimevamiwa na maharamia mbalimbali ambao wamekuwa wakikata misitu na kuchoma moto ovyo kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ya kijiji hali ambayo imekuwa ikitishi ukame na kuathiri upatikanaji wa mvua.
Alisema licha ya jitihada mbalimbali wanazofanya za kuhakikisha wanadhibiti uharibifu wa maliasili hizo ikiwemo uvunaji wa mbao na wanyama wanaotoka pembezoni ya mbuga ya Serue zimeshindikana kutokana na mbinu mbalimbali zinazotumiwa na mahalamia hao kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ya kijiji hicho.
Naye Lucas Talimo,alisema kuwa maliasili hizo ambazo ni pamoja na madini wao kama wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakishindwa kufaidika nazo licha ya kuzilinda na badala yake wageni ndio wamekuwa wakijinufaisha nazo kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wa vijiji hivyo.
Aliomba Serikali kuingilia kati vinginevyo malisili hizo zinaweza kutoweka wakati wowote kutokana na vitendo vinavyofanywa na mahalamia hao katika kata hiyo .
Akizungumzia hilo,Waziri Kombani aliagiza Uongozi wa Serikali ya Wilaya ya Ulanga kupitia ofisi ya Maliasili wilaya kulishughulikia suala hilo mara moja ili kuzuia kutoweka kwa maliasili hizo zinazockuliwa kinyemela na mahalamia hao.


No comments:

Post a Comment