HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, September 11, 2012

Mahenge wapata Tsh. 42 Mil kwa ajili ya Mradi wa Maji

Na Senior Libonge, Mahenge


WAZIRI wa Maji Profesa Jumanne Maghembe ameahadi kutoa kiasi cha shilingi milioni 42 kwa ajili ya kukamilisha mradi wa maji katika Mji wa Mahenge uliopo katika tarafa ya vigoi  wilayani ulanga mkoani Morogoro.

Mji wa Mahenge  unakabiliwa na uhaba wa  maji kutokana na kutokana na miundombinu yake kuchakaa ulihaidiwa kumalizika kwa tatizo hilo  na Rais Jakaya Kikwete alipotembelea wakati wa ziara yake mapema mwaka 2009.

Katika kutatua tatizo hilo la maji,Rais Kikwete alitoa kiasi cha shilingi milioni 200 ili kujengwa kwa miundombinu ya maji ambapo ilibainika ili kukamilisha mradi huo kulikuwa kunahitajika kiasi hicho cha fedha.

Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya Wilaya ya Ulanga, iliyosomwa na kaimu mkuu wa wilaya hiyo  Prisca Shewali,Mbunge wa jimbo hilo la Ulanga Mashariki  Celina Kombani alisema  kuwa wizara ya maji imeahidi kulimaliza tatizo la maji kwa kuleta fedha za kumalizia  mradi wa ujenzi

Alisema pamoja na mradi huo kuongezeka gharama lakini waziri wa maji Profesa  Jumanne Maghembe amuahidi kuwa mara fedha zitakapoingia wizarani kwake kipaumbele kitakuwa ni katika mji wa mahenge.

Kombani ambaye pia ni Waziri wa  nchi, Ofisi ya Rais Menejamenti ya Utumishi wa Umma,alisema kuwa kupatikana kwa fedha hizo kutawezesha kukamilisha kabisa mradi huo mkubwa wa maji na hivyo kumaliza kabisa tatizo hilo la ukosefu wa maji.

Awali akitoa taarifa ya ujenzi wa miundombinu ya maji ambayo inaendelea kujengwa katika maeneo mbalimbali ya tarafa ya vigoi mhandisi wa maji wilaya ya ulanga  Patrice Jerome, alisema mpaka sasa wameshafikia katika hatua ya usambazaji wa mabomba ambayo yamekamilika katika maeneo mbalimbali.

Mradi huo wa maji uliahidiwa na Jakaya Kikwete wakati wa ziara zake alizofanya wilayani Ulanga ambapo awali mradi huo ulikuwa ulikuwa na gharama ya shilingi milion 200 ambapo kwa sasa inadaiwa kupanda na kufikia shilingi milioni 300.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment