HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, September 10, 2012

MKUU WA WILAYA AWATAKA WANANCHI KUTOA TAARIFA SAHIHI

Na Henry Bernard Mwakifuna- IFAKARA


Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Bwana Hassani Masala amewataka wakazi wa Kilombero kuacha kutoa taarifa zisizo na ukweli kuhusu uhamaji wa maeneo Tengefu ya Bonde la Kilombero na  atakaye kamatwa  anatoa taarifa za uongo kuhusiana na kuhama kwa wavamizi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Bwana Masala amesema hayo wakati akifunga  Mdahalo wakukuza uwajibikaji wa Viongozi na Wawakilishi  wa Wananchi kwa Jamii  ulioandaliwa na Mtandao wa Azaki Mkoa wa Morogoro {UNGO}kwa kushirikiana na The Foundation for Civil Society uliofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Vijana(John Paul II ) uliopo mjini Ifakara.

Ametoa tahadhari hiyo kwa baadhi ya wananchi na viongozi wanaowapotosha wananchi juu ya zoezi la kuhama kwa wavamizi wa maeneo ya hifadhi na kuondolewa kwa mifugo vamizi.

 Wakati huo huo Mkuu huyo wa Wilaya ya Kilombero amewapongeza UNGO kwa kutoa Elimu kupitia mdahalo huo na amewaomba  kuzidi kutoa ushirikiano kwa serikali kwa kuleta maendeleo na kutoa Elimu kuhusu utawala bora kwa viongozi na wananchi.

Wakitoa mada ya utawala wa uwajibikaji katika  Usimamizi na Menejimenti ya Rasilimali katika sekta ya Maliasili Bwana Masanja Joram na Christer Njovu wamesema kuwa katika utawala na uwajibikaji kiongozi anatakiwa kuwa mvumulivu wakati watu wanatoa maoni katika mkutano au vikao na pia anatakiwa kukosoa au kukosolewa bila ya kuoneana aibu. Wawezeshaji hao pia wamewataka wananchi kujihusisha kusimamia maeneo ya Uvuvi ili kuzuia uvuvi haramu katika sekta ya maliasili.

No comments:

Post a Comment