HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Monday, September 10, 2012

MALALAMIKO 35 YAFIKISHWA TAKUKURU

Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa [TAKUKURU] Wilayani Kilombero imepokea  jumla ya malalamiko 35 kutoka sehemu mbalimbali za Wilaya hiyo katika kipindi cha mwezi Januari hadi Agosti mwaka huu ambayo hadi sasa yanaendelea kufanyiwa kazi katika hatua mbalimbali za kiuchunguzi.                                                                                          

Taarifa  iliyotolewa  kwa Waandishi wa Habari na Afisa wa Takukuru Bw.Festo Mdede  imeeleza kuwa  hadi  sasa kuna kesi tano [5]za kukamatwa na Rushwa ambazo bado zinaendelea kusikilizwa Mahakamani.

Mbali ya Kesi hizo Afisa huyo amesema kuwa Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa [w]Kilombero inatarajia kutoa elimu kwa wananchi ili kuwajengea ujasiri wa kutoa ushirikiano katika suala la kuzuia na kupambana na Rushwa ndani ya Wilaya hiyo.
  
Hata hivyo amesema kuwa mbali na kutoa elimu kwa wananchi taasisi imejiwekea mikakati ya  kufanya Warsha fupi ili  kupokea mawazo na ushauri  kutoka kwa wananchi kwa lengo la  kujenga ushirikiano utakao- saidia kurahisisha kazi ya kuzuia na kupambana na Rushwa .

Ametoa Wito kwa Wafanyakazi wa nyanja mbalimbali kufuata sheria za kazi  na kutoruhusu kutoa wala kupokea Rushwa bali ni kupambana kikamilifu  kuzuia Rushwa  ili wawe mfano mzuri na wa kuigwa katika jamii.

No comments:

Post a Comment