HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, September 13, 2012

Wananchi Ifakara watakiwa kuchangia ujenzi wa Sekondari

Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero.

Diwani wa Kata ya Ifakara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero Bwana Ramadhani Kiombile amesema suala la  kuchangia  shilingi Elfu Tatu Ujenzi wa Sekondari ni la Lazima na siyo la Hiyari.

Amesema kuwa Maendeleo ya eneo lolote yanaletwa na Kodi na Michango kama hiyo huku akiwataka Viongozi kuwajibika ili kufikia malengo waliyojiwekea.

Mchango wa Sekondari kwa Hiyari katika Kata ya Ifakara Mwisho kwa Shilingi Elfu Tatu ni Septemba 30 ambapo kuanzia Oktoba Mosi yeyote atakayebainika hajalipa atatozwa Faini ya Shilingi Elfu Kumi na Fedha halali Elfu Tatu jumla ikiwa ni Elfu Kumi na Tatu.

Kauli ya Bwana Kiombile aliitoa katika Kikao cha Baraza la Maendeleo la Kata ya Ifakara liliokaa katika Ukumbi wa Kantini Ifakara mbele ya Viongozi wa Vitongoji na Vijiji ambapo Diwani huyo amesema kuwa Wananco bado hawajaonesha Ushirikiano wa Dhati katika suala la Uchangiaji wa Mchango huo.

Kwa upande wake Diwani wa Viti Maalum Tarafa ya Ifakara Bi,Nasra Ngwega amewataka Watendaji na Wenyeviti wa Vitongoji kuwahamasisha wananchi mapema ili kuwaepusha na suala  kutozwa faini. Amesema hamasa inatakiwa ili Wanachi watoe Michango yao kwa Hiyari ili kuwaepusha na kukamatwa na Kutozwa Faini kitu ambacho kinawezekana kufanyika kabla ya Tarehe ya Mwisho ya Kuchangia kwa Hiyari.

 

No comments:

Post a Comment