HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, September 13, 2012

Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero

KASIMU HASSAN NJOHOLE (70), aliyekuwa Mmiliki wa Bendi ya NJOHOLE JAZZ BEND amefariki Dunia  hana katika Hospitali ya  Rufaa ya Mtakatifu Fransis Ifakara saa nanane Septemba 11 na anataraji kuzikwa leo.

Kwa muujibu wa Tarifa ya Hawa Njohole ambaye ni Dada wa Marehemu amesema kuwa Marehemu amekutwa na Mahuti baada ya kuugua kwa muda mrefu hi mbalimbali ambapo alikuwa amelazwa katika Hospitali hiyo  tangu majuzi.

Kasimu Njohole aliwahi kuimiliki Bendi yake iliyojulikana kwa jina la New Ifakara Jazz Band ambapo mashabiki kutokana na umahiri wake wakaibadilisha jina na kuuita Njohole Jazz Bendi mwaka 1960.

Mbali ya kumiliki Bendi Kassimu Njohole aliwahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero kati ya  mwaka 2000 hadi mwaka 2005.

 Hawa amesema mwaka 1984 hadi mwaka 1988 Marehemu alikuwa anaonesha sinema sehemu mbalimbali nchini Tanzania, na mwaka 1988 hadi mwaka 1990 alijiunga na Siasa na Mwaka 1994 alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Serikali ya Kitongoji cha Lipangalala. Mwaka 2000 alichaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Ifakara na alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kiolmbero hadi Mwaka 2005.

Mwaka 2006 alichaguliwa na uongozi wa CCM ngazi ya Wilaya kuwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilombero kwa muda wa miaka miwili badala ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilombero Bwana Kassimu Kulolela kufariki dunia. Bi Hawa Njohole amesema Mwaka 2008 aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Maji  Wilaya ya Kilombero hadi kifo chake. Marehemu ameacha Watoto Sita wakiume  watatu na wakike watatu.

Marehemu Kassimu Hassan Njohole atazikwa leo Septemba13 majira ya saa kumi jioni katika Makabuli ya ukoo waNjohole yaliyopo nyumbani kwake.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU, MAHALA PEMA PEPONI- AMINA

No comments:

Post a Comment