HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, September 13, 2012

Makundi makubwa ya Mifugo yaondoka Ulanga/Kilombero

Na Senior Libonge,Kilombero

MAKUNDI makubwa ya  mifugo yameanza kuondoka katika bonde la Mto Kilombero wakitekeleza agizo la serikali la kutaka mifugo yote iliyovamia katika bonde hilo kutolewa kwa hiari kabla ya nguvu za dola kuanza kutumika hapo Septemba 7 mwaka huu.


Nimeshuhudia malori makubwa yakiwa yamebeba mifugo huyo katika mji wa Ifakara tayari kwa safari ya kusafirisha mifugo hiyo na kuipeleka kusini mwa Tanzania kwenye mkoa wa Lindi ambapo serikali imetenga eneo maalum la kuishi mifugo.

Juzi viongozi wa wilaya zote mbili za Kilombero na Ulanga walikuwepo mjini Ifakara tayari kwa kuruka na ndege ndogo iliyoletwa na serikali kwa ajili ya kukagua mifugo ama wakulima waliobaki katika maeneo yaliyopigwa marufuku kuwepo na kweli zoezi hilo lilifanyika kwa umakini.

Katika ziara hiyo timu hiyo iliyoongozwa na mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala na yule wa Ulanga Francis Miti walitembelea bonde lote la Kilombero ili kujionea uharibifu uliofanyika na kwa kiasi kikubwa walibaini kuwa mifugo mingi imeondoka katika bonde hili isipokuwa kwa wafugaji wachache ambao wamejifanya kuificha mifugo yao katika baadhi ya misitu ndani ya bonde hilo.

Baada ya kumaliza kuzungukia bonde hilo wakuu hao wa wilaya walisema kuwa operesheni ya kuwaondoa wafugaji hao imekwisha anza na zoezi linalofanyika hivi sasa ni viongozi wa vijiji na vitongoji kuwahamasisha wafugaji wote waliokuwepo maeneo hayo kuondoa haraka mifugo yao na kubakia ile mifugo halali inayotakiwa kubaki maeneo hayo.

Mifugo halali ni ile iliyowekwa alama na ambayo imekubalika na wananchi wa kijiji husika kuwepo maeneo hayo hasa kwa kuzingatia ukubwa wa eneo husika na mahitaji halisia ikiwemo ya ng’ombe wa kilimo(maksai).

Kwa sasa mifugo mingi imebainika ipo pembezoni mwa milima ya Udzungwa katika tarafa ya Mlimba ambapo haijajulikana kuwa wafugaji hao wameificha mifugo yao maeneo hayo ama wapo njiani kuisafirisha kuipeleka mikoa ya Iringa na Mbeya.

Hata hivyo wafugaji hao wavamizi sambamba na wakulima walioingia katika maeneo ya hifadhi wamepewa tahadhari kuwa kauli ya serikali ipo palepale ya kutaka wote watoke maeneo hayo ukizingatia kuwa serikali haitaki kutumia nguvu kuwaondoa ukizingatia kuwa ni wananchi halali wan chi hiyo.


Ila taarifa imesema kuwa serikali haitashindwa kutumia nguvu kuwaondoa wavamizi hao kama wakiendelea kukaidi agizo la kutaka kutoka eneo hilo ukizingatia mpango wa serikali hivi sasa ni kuliona bonde la Kilombero likirudi katika hali yake ya zamani ya kuwa na ardhioevu kwa ajili ya kilimo na hifadhi tofauti na hivi sasa ambapo asilimia kubwa ya bonde hilo limeharibika kutokana na uvamizi wa mifugo na wakulima.

No comments:

Post a Comment