HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Friday, September 21, 2012

Wananchi Kjiji cha Kivukoni wataka mapato ya Geti za mazao

Na Senior Libonge,Ulanga

WAKAZI wa kijiji cha Kivukoni wilayani Ulanga wameiomba halmashauri ya wilaya kukipa upendeleo kijiji hicho kwa kuwapatia asilimia ya mapato ya kizuizi cha wilaya kilichopo katika kijiji chao ili kufanyia shughuli mbalimbali za maendeleo.

Rai hiyo wameitoa juzi wakati wa mafunzo ya ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali za umma sekta ya kilimo wilaya ya Ulanga yanayotolewa na asasi isiyo ya kiserikali ya kikundi cha wanawake wa St.Maria Magdalena ya mjini Ifakara.

Wananchi hao wamesema kuwa hivi sasa kijiji hicho kinapata asilimia chache ya mapato licha ya kizuizi hicho kuwepo kwenye kijiji chao na wao kuendelea kuwa maskini huku wakishindwa kujiendesha ikiwemo wenyeviti wa vitongoji kukosa fedha za shajala.

Wamesema kwa hivi sasa hawaoni faida ya kuwepo kizuizi hicho katika kijiji chao kwani wamekuwa wakijichangisha wao wenyewe michango mbalimbali ya maendeleo bila kupata msaada wa kutosha katika halmashauri ukizingatia kuwa sehemu nyingine zenye kitegauchumi cha wilaya kijiji husika upata mafanikio ya mradi uliopo.

Aidha wananchi hao wamewaomba wabunge wa majimbo yote ya Ulanga mashariki na magharibi kufanya mikutano kwenye kijiji chao kwani wao ukipita tu kijiji hicho punde waingiapo katika ziara zao kwenye majimbo yao ukizingatia kuwa kijiji hicho ndiyo mlango wa wilaya ya Ulanga.

Kuhusu pembejeo za ruzuku za kilimo wananchi hao wamesema kuwa licha ya kuchelewa kufika kwa wakati pia pembejeo hizo zimekuwa bei ghali na hali hiyo umfanya mkulima wa chini kushindwa kuipata na kutimiza malengo yake katika kilimo..

Kwa upande wake afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw Josephat Masanyoni ili kupata ukweli kuhusu malalamiko ya wananchi ambapo alikiri kweli kuwa malalamiko ya wananchi hao ni ya msingi na kuelezea suala la mbolea kuwa kweli ilichelewa kufika na licha ya kufika baadhi ya wananchi walikosa na tatizo kubwa ni uchangiaji wa fedha toka kwa wananchi.

Masanyoni akielezea suala la mapato ya kizuizi alisema kweli hawana asilimia wanayopata kutoka kwenye kizuizi hicho licha ya wao kupeleka malalamiko kwa viongozi wa wilaya na hata wananchi kutoa malalamiko yao punde wanapokuja viongozi mbalimbali.

Kwa upande wake mratibu wa mafunzo hayo  Christina Kulunge amesema mafunzo hayo ni ya siku 5 yanafanyika katika kata za Kivukoni,Minepa na Lupiro na lengo lake ni kuwajengea uwezo wananchi kuhusu ufuatiliaji wa pembejeo za ruzuku katika sekta ya kilimo.

Amesema pia wananchi wanatakiwa kuwa na ufahamu wa uchangiaji wa serikali katika mbolea za ruzuku na maadili ya utawala bora.

Christina amesema mradi huo ni wa mwaka mmoja na una gharama ya shilingi milioni 43 ambazo zimefadhiliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya The Foundation for civil society

No comments:

Post a Comment