HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Thursday, September 6, 2012

Na Senior Libonge,Kilombero
VIJIJI 6 wilayani Kilombero vimekabidhiwa vifaa vya uendeshaji wa vitalu vya miti na bustani ya mbogamboga vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 6 kutoka asasi inayojishughulisha na uhifadhi wa mazingira na maendeleo katika bonde la Kilombero(KIVEDO).
 Akikabidhi vifaa hivyo katibu mtendaji wa KIVEDO Hamza Kaposa amevitaja vijiji vilivyokabidhiwa vifaa kuwa ni Namwawala,Mofu,Kisegese,Mbingu,Mkangawalo na Udagaji lengo ni kukabiliana na tatizo la mabadiliko ya tabia nchi.
 Kaposa amesema ili kufanikisha lengo hilo,KIVEDO kwa kushirikiana na vijiji hivyo vya mradi wataanzisha bustani za miti sita yaani kila kijiji kuwa na bustani moja kwa kuotesha,kukuza na upandaji miti na pia kupitia ufadhili wa shirika la Plan International watatoa vifaa kwa ajili ya uendeshaji wa bustani ya miti katika vijiji.
 Katibu huyo amebainisha kuwa kila kijiji kinachukua jukumu la kuhakikisha kuwa vifaa vya mradi wa kusimamia na kuendeleza bustani ya miti vinatumika kwa lengo na madhumuni ya kutekeleza kazi za mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na siyo vinginevyo.
 Amesema kuwa sababu ya kuchagua vijiji hivyo ni kutokana na vijiji hivyo hapo nyuma kufanyiwa utafiti na kugundulika vimeathirika na mabadiliko ya tabia nchi tokana na wananchi kutegemea kilimo na uvuvi katika maeneo hayo na pia wameona kuwa hatua zinazochukuliwa katika vijiji hivyo vitaleta mafanikio ya haraka tofauti na maeneo mengine.
 Kaposa amesema ili kijiji kikabidhiwe vifaa vya kuendesha bustani ya miti kitalazimika kuwasilisha majina ya wanakijiji waliojitolea kuitunza na kuendesha bustani ya miti ili miti itakayozalishwa igawiwe kwa wanakijiji kwa ajili ya kuipanda mashambani,maeneo ya makazi na kwenye vyanzo vya maji na kingo za mito.
 Aidha kijiji kinatakiwa kutenga eneo la ardhi kwa ajili ya kuanzisha eneo la kitalu cha bustani ya miti,iwe kwenye eneo la kijiji,taasisi ya serikali au mtu binafsi na gharama za utunzaji wa kitalu cha miti itakuwa ni jukumu la kijiji kwa kushirikiana na watu watakaokuwa tayari kujitolea kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.
 Vifaa vilivyokabidhiwa vijiji hivyo ni pamoja na Matoroli,makoleo,viriba vya plastiki,visu,sprayer,ndoo,majembe,reki,watering cane,mapanga,mafyekeo,mifuko ya mbolea ya kukuzia na garden foxes.
 Shirika la KIVEDO linatekeleza mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwa muda wa miaka mine kwa ufadhili wa shirika la Plan International na pamoja na mambo mengine mradi unajikita katika shughuli za uhifadhi wa mazingira na maliasili na kuboresha upatikanaji wa mazao na masoko yake.

No comments:

Post a Comment