HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, November 27, 2012

LUPIRO KUNUFAIKA NA MRADI MKUBWA WA MAJI


Na Senior Libonge,Ulanga

Wananchi wa kijiji cha  Lupiro  chenye wakazi zaidi 4000 wilayani Ulanga mkoani Morogoro wanategemea kunufaika na mradi mkubwa wa maji unaofadhiliwa na benki ya Dunia.

Akiongea wakati wa ziara ya Madiwani wa kamati ya Fedha Utawala na Mipango kutembelea miradi ya maendeleo Mhandisi wa Maji Wilaya ya Ulanga  Patrice Jerome amesema benki ya dunia imetoa kiasi cha Tshs milioni 233 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji Lupiro ambapo miundombinu ya maji ,tanki la kuhifadhia maji na ujenzi wa vituo 20 vya maji vya  jumuiya ,ufungaji wa mabomba ya maji , ujenzi wa pampu house na ufungaji wa pampu ya kusukuma maji .

Jerome amesema kuwa tanki linalojengwa litakuwa na uwezo wa kuhifadhi lita za ujazo 90 za maji (sawa na lita 90,000) na kuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa tarafa hiyo kwani eneo hilo lina uhaba mkubwa wa maji kwa muda mrefu.

Amesema mradi huu ni miongoni wa miradi ya vijiji 10 vinavyotarajiwa kujengwa kupitia pragramu  hii ya maji na usafi wa mazingira.

Nao wajumbe wa kamati waliwashukuru benki ya dunia kupitia program ya maendeleo ya sekta ya maji kwa kufadhili mradi huo kwani itawasaidia wananchi na kuwasihi wananchi  kutunza na kuhifadhi vizuri mradi huo pindi utakapokamilika ili uwe endelevu na kufikia lengo la kuanzishwa kwa mradi huo.

 Kamati imesisitiza kuanzishwa  na kusajiliwa kwa jumuiya hiyo ya watumiaji maji sambamba na kuwa na mfuko wa maji kwa ajili ya kuendesha mradi huo.Pia miradi mingine kama Igota kichangani  na Gombe ifuatiliwe kwani taratibu za manunuzi  zilishakamilika ili ianze kujengwa .

Akizitaja changamoto zinazojitokeza katika ujenzi wa mradi huo mshauri wa mradi Bw Raymundi wa kampuni ya ushauri ya Interconsult  ya Dar  es salaam amesema kuwa ni ugumu wa upatikanaji wa vifaa vya ujenzi na uhaba wa upatikanaji wa vibarua ambapo wengi wao wanadai maslahi makubwa kuliko fedha iliyopangwa.

Ziara ya kamati ya Fedha Utawala na Mipango pia ilitembelea miradi mbalimbali katika tarafa za Vigoi,Lupiro na mradi mkubwa wa umwagiliaji unaoanza kujengwa katika kata ya Minepa.

No comments:

Post a Comment