HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Sunday, November 4, 2012

MILIONI 544 ZAKUSANYWA KAMA USHURU JULAI-SEPTEMBA WILAYANI KILOMBERO


Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero.

JUMLA ya Shilingi Milioni 544 sawa na Asilimia 84.8 ya lengo zimekusanywa na Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero  kutokana na Ushuru katika kipindi cha Mwezi Julai hadi Septemba mwaka huu huku lengo likiwa ni kukusanya Shilingi Milioni 647.

Taarifa ya Kamati ya Fedha iliyotolewa katika Kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi hivi Karibuni imeeleza kuwa ukusanyaji wa ushuru katika wilaya hiyo umeshuka .

Katika kipindi cha Julai hadi Septemba mwaka huu, Halmashauri hiyo imekusanya ushuru kutoka kampuni ya Kilombero Plantation Limited (KPL)  iliyopo kata ya Mngeta shs. milion 16 tu wakati lengo lilikuwa kukusanya shs. milion 30 kila mwezi.

Taarifa hiyo imezidi kueleza kwa upande wa Minada katika kipindi hicho Halmashauri hiyo imekusanya ushuru shs. milion 2 tu, lengo lilikuwa kukusanya shs. milion 7, ushuru wa Soko imekusanya shs. milion 3 wakati lengo ilikuwa kukusanya shs. milion 23, ushuru wanyumba za kulala wageni imekusanya shs. milion 17,748,050 ni sawa na asililimia 17 lengo lilikuwa kukusanya shs. milion 98,776,000|= na ushuru wa miwa imekusanya shs. milion 18 ni sawa na asilimia 14 lengo lilikuwa kukusanya shs milion 127.

Wakati huo huo Wajumbe wa Baraza hilo wamewataka Maafisa Watendaji wa Kata 21 waliopo katika Wilaya ya Kilombero kufanya kazi ya ziada ya kukusanya ushuru ili kuiletea mapato makubwa Halmashauri hiyo ili iweze kuleta maendeleo kutokana na miradi inayopangwa kutekelezwa.

Wamesema Watendaji wa Kata mwishoni mwa mwaka jana wamepewa Pikipiki ili kufuatilia ukusanyaji wa ushuru katika kata zao lakini matokeo yake mapato yatokanayo na ushuru yameshuka.

Kati ya Kata 21, Kata za Idete na Mofu kwa muujibu wa Taarifa ya Kamati ya Fedha  hazikufanya Vizuri katika Zoezi la Ukusanyaji Ushuru katika Kipindi hicho cha Julai hadi Septemba.

Mbali ya hilo Wajumbe wa Kamati ya Fedha wametakiwa kubuni mbinu mbadala ya kuingizia mapato Halmashauri ya Wilaya, huku kamati hiyo ya Fedha ikitoa Pendekezo la  kulirudisha geti la Idete ili mapato yaweze kuongezeka, lakini wajumbe wa Baraza hilo wamekataa pendekezo hilo.

No comments:

Post a Comment