HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Sunday, November 4, 2012

KITONGOJI CHA IFAKARA CHAVUKA LENGO MICHANGO YA MAENDELEO


Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero

Kitongoji cha Ifakara mjini katika Kipindi cha Julai hadi Oktoba kimevuka lengo kwa ukusanyaji wa michango ya maendeleo kutoka kwa jamii kwa muujibu wa Taarifa ya Kamati ya Maendeleo ya Kata.

Taarifa ya Michango ya Maendeleo ya Kata ya Ifakara Mjini kwa mwaka huu, iliyotolewa katika kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata(KMK) cha Hivi Karibuni, imeeleza kuwa kitongoji cha Ifakara mjini Kimepangiwa kukusanya michango ya maendeleo kutoka kwa Jamii shs.4,776,000/= kutoka nguvu kazi 1,592 iliyopo, lakini iimekusanya jumla ya shs.4,974,000/=na kuvuka lengo la shs.198,000/=.

Taarifa hiyo imezidi kueleza kuwa kitongoji cha Mkuya kimekusanya mchango  wa maendeleo kutoka kwa jamii shs. 1,806,000/= wakati lengo walilopangiwa ni kukusanya shs.1,812,000/= kutoka nguvu kazi 604 iliyopo katika kitongoji hicho.

Kitongoji cha Nduna kwa Muujibu wa Tarifa,hakijafanya vizuri katika zoezi la ukusanyaji wa Michango ya Maendeleo, ambapo lengo wamepangiwa kukusanya shs.5,235,000/= kutoka nguvu kazi 1745 iliyopo katika kitongoji hicho, lakini imekusanya jumla ya shs.2,766,000/= na inadaiwa shs.2,469,000/= ambazo bado hazijachangwa.

Taarifa inaonesha Kitongoji cha Nduna kina nguvu kazi 823 ambayo bado haijachangia michango yao ya Maendeleo hadi kufikia Oktoba 15 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment