HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Sunday, November 4, 2012

MILIONI 81 KUWANUFAISHA WAKAZI WA KILOMBERO


Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero.

WANACHAMA 927 wa Mfuko wa Mzunguko wa Shirika lisilo la Kiserikali la Camfed wana akiba ya  jumla ya Shilingi 81,964,000 ambazo zipo kwa ajili ya kukopeshana.

Bi.Tukaeje Habibu, Afisa Mradi Camfed Tanzania, akitoa Taarifa ya Mwaka ya Mfuko wa Mzunguko amesema Wanachama hao wana Jumla ya Shilingi Milioni 32.4 na Camfed imewapatia msaada wa Shilingi milioni 49,520,000.

Amesema kuwa mfuko huo umeweza kuwanufaisha Wanachama kutoka Wilaya Kumi nchini Tanzania na tayari wanachama wameanza kuchukua Mikopo kutoka  kwenye Mfuko huo.

Ameongeza kuwa changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni baadhi ya Viongozi wa Vikundi vinavyofadhiliwa na Shirika hilo kula fedha huku akizitaja Wilaya za Kilolo, Kilosa na Kilombero zikiongoza kwa Utafunaji wa Fedha hizo.

Kwa upande wa Kilolo Viongozi Watatu wametafuna Jumla ya Shilingi Milioni 2,140,000, kwa upande wa Kilombero kiongozi mmoja ametafuna 453,000 na  Kilosa kiongozi mmoja ametafuna Laki 190,000. 

Kwa upande wake Nasikiwa Duke, Afisa Mradi wa Young Women wa Shirika la Camfed akitoa Ripoti ya Mwaka amesema kuwa Shirika hilo mpaka sasa linafanya kazi na Shule 540 likiwa na Miradi aina mbili ambayo ni kumsaidia Mtoto wa Kike na kumwendeleza kiuchumi.

Viongozi hao wa Camfed Shirika lenye Makao Makuu Nchini Uingereza linalofanya kazi na Nchi Tano kwa sasa ikiwemo Tanzania waliyasema hayo walipokuwa katika Mkutano wa Mwaka uliofanyika Ifakara, Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro na kuhudhuriwa na Wanachama kutoka Wilaya Kumi nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment