HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, December 4, 2012

Utunzaji wa Mazingira sawa, Haki za Binadamu Je?


Na Senior Libonge,Ulanga

SERIKALI  imetakiwa kuhakikisha inafanyia marekebisho sheria za ardhi zilizopo, ili mashauri yanayohusu migogoro ya ardhi yaweze kushughulikiwa kwenye ngazi za vijiji na kata ardhi hizo zilipo badala ya kupeleka mashauri hayo ngazi za wilaya, mahakama kuu ama za rufaa, ambapo wakati mwingine imewafanya wananchi kupoteza haki zao kwa kushindwa kumudu gharama kubwa za uendeshaji.





Ushauri huo ulitolewa kwa nyakati tofauti na Wananchi na viongozi wa Tarafa za Malinyi na Ruaha wilayani Ulanga Mkoani Morogoro, wakati wakichangia kwenye midahalo kuhusu uwazi na Uwajibikaji katika sekta ya ardhi, iliyoandaliwa na Umoja wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali wilayani Ulanga (UNGOKI) kwa ufadhili wa shirika la Foundation For Civil Society ambapo walitolea mfano iwapo ardhi hiyo itakuwa ikigombewa baina ya mwananchi wa kawaida na mwekezaji mkubwa, ni rahisi kwa mwekezaji kushinda shauri husika kutokana na uwezo mdogo wa mwananchi kufuatilia shauri husika kama inavyotakiwa na kukosa wazi haki zake stahili.



Wananchi hao pia walilalamikia mabaraza ya adrhi ya vijiji na kata kukosa nguvu za kisheria katika kushughulikia migogoro, hivyo kudharaulika katika maeneo yao, ambapo iwapo mlalamikiwa ataitwa na baraza hilo na kushindwa kufika, mabaraza hayo yamekosa nguvu kuwachukulia watuhumiwa hatua.

Katika midahalo hiyo ambayo kauli mbiu yake ilikuwa ni “Uwazi na Uwajibikaji ni msingi wa maendeleo,wananchi hao walilalamikia mashauri ya ardhi kuandikwa kwa lugha ya kiingereza katika baraza la ardhi na nyumba, changamoto za mipaka katika vijiji vyao, wananchi kushindwa kushirikishwa katika masuala ya ardhi ikiwemo kupitisha majina ya watu wanaoomba maeneo, na gharama kubwa ya kufuatilia mashauri hasa yale yanayofikishwa ngazi za juu kama baraza la wilaya, mahakama kuu na mahakama ya rufaa.





Baadhi ya wananchi hao Omary Ibrahim, Stephen Kasasi,Dvodius Mlungachuma,Edward Lupogo na Agnes Mpangule walilalamikia wageni kupewa ardhi tena maeneo makubwa katika maeneo yao, bila kushirikisha ugawaji huo katika mikutano ya vijiji, jambo linalowanyima haki wakazi husika,na viongozi wengine kutumia nyadhifa zao kujimilikisha maeneo makubwa, jambo linalochochea migogoro miongoni mwa wananchi.

Aidha Stephen Kasasi Lugumey na wenzake kutoka Kijiji cha Makelele walilalamikia eneo lao la kijiji kuwa dogo na hivyo kushindwakufanya matumii bora ya ardhi, ikilinganishwa na vijiji vidogo, hivyo kuhoji ukubwa wa eneo la kijiji unapaswa kuwa vipi na kwamba ni vyema vijiji vikapimwa upya na kugawanywa kwa mlingano ulio sawa. .

Nao wanavijiji wa Tarafa ya Ruaha, Kanusian Nkasi,Medist Zimani,Todros Katanda,Ezekiel Maridadi,Renfrida Pesa na Williama Kologati, pamoja na kulalamikia madai kama yalivyojitokeza Malinyi, walihoji mpango wa matumizi bora ya ardhi kuchelewa kufanywa sasa, kutokana na kuwa tayari wananchi wameshajimilisha maeneo na kutishia ubora wa mpango huo.




Wakitoa mada kwa nyakati tofauti katika midahalo hiyo, Mratibu wa UNGOKI, Maiko Chami,mjumbe wa umoja huo Ansagar Kwanja na mtoa mada Mohamed Nguku,waliwaasa wananchi kushiriki mikutano ya vijiji ili kutoa mapendekezo, maoni na ushauri juu ya bajeti za vijiji, mpango wa matumizi bora ya ardhi na changamoto na mahitaji mengine muhimu yanayoyakabili maeneo yao.

Chami aliwashauri kutokana na ufinyu wa bajeti ya serikali kuwezesha kufanya matumizi bora ya ardhi kufikia vijiji 38 kati ya 91 vya wilaya ya Ulanga, ni vyema vijiji vingine vikapitisha maamuzi ya kutaka mpango huo kwenye mikutano yao ya vijiji na hata kuomba wahisani na mashirika mbalimbali kusaidia uwekaji wa mipango hiyo, badala ya kuisubiri Serikali, huku akihimiza ushirikishwaji kuwa ni njia pekee na kubwa ya kutatua migogoro ya ardhi.

“Migogoro hii ya ardhi ikitatuliwa vijijini ni jambo zuri na jepesi kutatulika, kwa sababu ardhi ipo kwenu, kuliko kupeleka migogoro hii ngazi za juu, ni kweli bado kuna changamoto ya sheria za ardhi, kama kushindwa kutoa nguvu kisheria kwenye mabaraza ya ardhi ya vijiji na kata, ambapo mlalamikiwa asipotokea kwenye shauri, baraza limekuwa likikosa nguvu kisheria kumchukulia hatua,lakini bado wanaharakati wanalipigia kelele”Alisema Mratibu huyo wa UNGOKI akijibu madai mbalimbali ya wananchi hao.

Nguku alisema halmashauri za vijiji hazina Mamlaka kisheria kugawa maeneo, na wanaopaswa kufanya hivyo ni wananchi kupitia mikutano ya vijiji huku akiwatahadharisha kuwa makini na ugawaji wa maeneo makubwa kwa wawekezaji, kwani wana hatari ya kukosa haki mbeleni iwapo wanaopewa maeneo watapata hati miliki na kutumia sheria hizo hizo za ardhi kuwalinda.

Wananchi walipitishwa katika mada mbalimbali ikiwemo sheria za ardi namba nne na tano za mwaka 2004, sheria ya kijiji ya mwaka 1999, historia ya uwepo wa sheria za ardhi,migogoro inayojitokeza vijijini na mifumo inayotumika katika utatuzi na mpango wa usimamizi na matumizi bora ya ardhi.

No comments:

Post a Comment