HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Saturday, December 1, 2012

Jumla ya shilingi milioni 212,886,000 zakusanywa katika zoezi la kuondoa mifugo Bonde la Mto Kilombero


Na Senior Libonge- Ifakara

JUMLA ya shilingi milioni 212,886,000 zimepatikana ikiwa ni mapato ya uwekaji alama mifugo na faini katika zoezi la uondoaji mifuko katika bonde tengefu la Kilombero kwa wilaya ya Kilombero.

Akizungumza jana katika kikao cha kamati ya uashauri ya wilaya(DCC)Mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala amesema kuwa fedha hizo zimepatikana baada ya kuanza kwa zoezi la uwekaji alama lilianza Agosti 21 na kumalizika Septemba 30 mwaka huu na pia zoezi la faini kwa wafugaji waliokaidi amri halali lililoanza Oktoba 30 mwaka huu.

Masala amesema zoezi la kuweka alama mifugo inayostahili kubaki kulingana na ukubwa wa eneo husika lilihusisha vijiji vilivyopo ndani ya eneo la Ramsar na vilevile nje ya eneo hilo kwa kufanya mikutano mikuu ya hadhara kwa ajili ya utambuzi wa wafugaji halali na wanaotakiwa kubaki katika kila kijiji.

Alisema jumla ya ng’ombe 52,780 waliwekwa alama kwa gharama ya shilingi 1000 kwa kila ng’ombe na kupata jumla ya shilingi milioni 52,780,000 kama makusanyo ya zoezi hilo na kati ya hizo shilingi milioni 27,940,300 zilitumika kuendelea na zoezi hilo.

Amebainisha kuwa katika zoezi la uondoaji wa mifugo ambalo zoezi hilo bado linaendelea mpaka sasa jumla ya wafugaji 2,428 wenye ng’ombe wapatao 9,248 walitozwa faini kwa viwango mbalimbali kulingana na makosa waliyopatikana nayo.

Mkuu huyo wa wilaya amesema jumla ya ng’ombe 3,482 walitozwa shilingi 10,000 na kupatikana shilingi milioni 34.8 huku ng’ombe 5,379 walitozwa shilingi 20,000 na kupatikana shilingi milioni 107.5,ng’ombe 264 walitozwa shilingi 40,000 na kupatikana shilingi milioni 10.5 na hiyo inafanya shilingi milioni 152.9 kuwa jumla ya mapato yaliyotokana na faini.

Masala amesema hata hivyo zoezi utoaji wa vibali vya kusafiria lilienda sambamba na zoezi hilo ambapo idadi ya ng’ombe 4764 walipatiwa vibali kwa gharama ya shilingi 1500 na shilingi milioni 7.1 zimekusanywa kama ruzuku ya serikali kuu.

Amesema fedha zilizoidhinishwa katika zoezi la uwekaji wa alama ng’ombe na uondoaji wa mifugo katika bonde tengefu la Kilombero ni shilingi milioni 152.7 na fedha iliyotumika hadi sasa ni shilingi milioni 94 na kufanya salio la shilingi milioni 14.1.

Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya amesema zoezi la kuondoa mifugo linaendelea japokuwa linakabiliana na changamoto mbalimbali ambazo wataalamu wanaendelea kukabiliana nazo

No comments:

Post a Comment