HONGERA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

photos

Welcome to UCRC

About Me

Ulanga Community Resource Centre is a not-for-profit company limited by guarantee which was initiated with the aim of capacitating the resident peoples of Ulanga and Kilombero Districts and Tanzania in general to secure the right information and hold their duty bearers accountable in a bid to promote sustainable community development. UCRC as well aims at promoting educational activities in Ulanga District through facilitation of necessary educational resources in the area which include well equipped libraries and study centers. UCRC also works on land and natural resource rights for the marginalized rural people in Tanzania which also include sustainable use of such resources. It also provides legal aid and assistance to the poor, particularly women, children, the disabled and other disadvantaged groups in the society on different themes including land and gender.

Tuesday, January 1, 2013

SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA ULANGA COMMUNITY RESOURCE CENTRE

KARIBUNI MGANDU



Na Francis Uhadi

Ndugu wapendwa Taasisi yetu ya Ulanga Community Resource Centre inawatakia mafanikio mema katika mwaka huu mpya wa 2013.


Kwa upande wetu tumefurahi kwa kuwa tumeweza kusajili Taasisi hii ambayo tunadhamilia kuifungua rasmi mwaka huu. Kama tukiwa wakweli tukilinganisha nyumbani kwetu Ulanga, Kilombero na Morogoro kwa jumla watu wetu ni maskini sana ingawa wana rasilimali nyingi zinazowazunguka. 


Kadhalika, tofauti na maeneo mengine kama vile Kilimanjaro, Arusha, Mbeya, Mwanza na hivi karibuni Mkoa wa Pwani, Lindi, Mtwara nk imekuwa na amsha amsha sana ya asasi za kiraia na kutokana na kazi hizo elimu na uelewa wa watu umeongezeka sana ikiwa ni pamoja na kuwachagua watu wenye uwezo na kuwawajibisha pale inapobidi.


Masika inaingia sasa, yale magari yanayotusaidia kama Morobest na AlySaedy karibu yataishia Ifakara. Kwetu sisi kama Ulanga Community Resource Centre tunaamini kuwa wananchi wanapoelimishwa juu ya haki zao na kuwa na taarifa sahihi ndipo wanapoweza kuzidai haki hizo na huu ndio hasa msingi wa kuanzishwa kwa Ulanga Community Resource Centre.


Daraja la mto Kilombero hadi leo kazi bado haijaanza ingawa kumekuwa na taarifa kuwa mkataba ulikwisha sainiwa. Ni nani anapaswa kulifuatilia hilo na kuhakikisha linatekelezwa?


Vunguvugu hili linatakiwa lianzie kwa vijana, tunafikiri mijadala yetu kwa mwaka huu 2013  ijielekeze kwenye mustakabali wa jamii inayoteseka kwa kukosa maendeleo kule nyumbani.  Hata hivyo hatuta weza kufikia lengo hilo kama si kwa kushirikiana, mwaka huu 2013 uwe ni mwaka wa kushirikiana zaidi na kukosoana inapobidi.


Tusiishie kufanya mijadala ya Facebook bila utekelezaji kwa vitendo hasa kwa kule nyumbani Ulanga/Kilombero.  Mwisho tunawatakia mwaka mpya wenye Mafanikio tele.

         

         


No comments:

Post a Comment