Na
Senior Libonge,Ulanga
Wananchi
wa kijiji cha Lupiro chenye wakazi zaidi 4000 wilayani
Ulanga mkoani Morogoro wanategemea kunufaika na mradi mkubwa wa maji
unaofadhiliwa na benki ya Dunia.
Akiongea wakati wa ziara ya Madiwani wa kamati ya
Fedha Utawala na Mipango kutembelea miradi ya maendeleo Mhandisi wa Maji Wilaya
ya Ulanga Patrice Jerome amesema benki ya dunia imetoa kiasi cha
Tshs milioni 233 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji Lupiro ambapo miundombinu
ya maji ,tanki la kuhifadhia maji na ujenzi wa vituo 20 vya maji
vya jumuiya ,ufungaji wa mabomba ya maji , ujenzi wa pampu house na
ufungaji wa pampu ya kusukuma maji .
Jerome amesema kuwa tanki linalojengwa litakuwa na
uwezo wa kuhifadhi lita za ujazo 90 za maji (sawa na lita 90,000) na kuwa
msaada mkubwa kwa wakazi wa tarafa hiyo kwani eneo hilo lina uhaba mkubwa wa
maji kwa muda mrefu.
Amesema mradi huu ni miongoni wa miradi ya vijiji
10 vinavyotarajiwa kujengwa kupitia pragramu hii ya maji na usafi wa
mazingira.
Nao wajumbe wa kamati waliwashukuru benki ya dunia
kupitia program ya maendeleo ya sekta ya maji kwa kufadhili mradi huo kwani
itawasaidia wananchi na kuwasihi wananchi kutunza na kuhifadhi
vizuri mradi huo pindi utakapokamilika ili uwe endelevu na kufikia lengo la
kuanzishwa kwa mradi huo.
Kamati imesisitiza kuanzishwa na
kusajiliwa kwa jumuiya hiyo ya watumiaji maji sambamba na kuwa na mfuko wa maji
kwa ajili ya kuendesha mradi huo.Pia miradi mingine kama Igota kichangani na
Gombe ifuatiliwe kwani taratibu za manunuzi zilishakamilika ili
ianze kujengwa .
Akizitaja changamoto zinazojitokeza katika ujenzi
wa mradi huo mshauri wa mradi Bw Raymundi wa kampuni ya ushauri ya
Interconsult ya Dar es salaam amesema kuwa ni ugumu wa
upatikanaji wa vifaa vya ujenzi na uhaba wa upatikanaji wa vibarua ambapo wengi
wao wanadai maslahi makubwa kuliko fedha iliyopangwa.
Ziara ya kamati ya Fedha Utawala na Mipango pia
ilitembelea miradi mbalimbali katika tarafa za Vigoi,Lupiro na mradi mkubwa wa
umwagiliaji unaoanza kujengwa katika kata ya Minepa.
No comments:
Post a Comment