Henry Bernard Mwakifuna. Kisegese-Kilombero
JUMLA ya Shilingi Milioni 95,703,587 zimetumika kwa ajili ya Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kisegese kilichopo kata ya Idete katika Wilaya ya Kilombero.
Akisoma Taarifa ya Makabidhiano ya Zahanati ya kijiji cha Kisegese mbele ya Mgeni Rasmi Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero Bwana Evarist Mmbaga, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Milima ya Udzungwa Bwana Vitalis Peter Uruka amesema Shirika la Hifadhi ya Taifa Tanzania (TANAPA) kupitia Hifadhi hiyo limechangia jumla ya Shilingi Milioni 87,042,320 katika ujenzi pamoja na Uwekaji wa Samani na Vifaa Tiba.
Amesema Mchango wa jamii katika mradi huo Zahanati ni Shilingi Milioni 8,661,267.
Ujenzi wa Zahanati hiyo umefanyika kwa Ushirikiano wa Jamii na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero kupitia Idara za Afya na Uhandisi.
Ameongeza kuwa uwepo wa Zahanati hiyo ni utekelezaji wa Sera ya Serikali ya kutoa Huduma ya afya hivyo Jamii watanufaika kwa kupunguza umbali wa Wagonjwa kutembea kufuata Huduma za Matibabu.
Kuboresha na kuinua kiwango cha Afya hasa katika Huduma ya Mama Wajawazito kupata Huduma na kujifungua salama na kuwawezesha Wagonjwa kupata Matibabu mapema kwa Maradhi yanayoweza kutibika.
Bwana Vitalis ameongeza kuwa uwepo wa Zahanati hiyo ya Kisegese utaongeza ari na Tija kwa Wananchi kuwawezesha kufanya shughuli za kimaendeleo na za kujiongezea kipato kama kilimo, Biashara na hivyo kuinua uchumi wao.
Hifadhi ya Milima ya Udzungwa ni Mojawapo ya Hifadhi 16 zinazosimamiwa na Shirika la Hifadhi ya Taifa(TANAPA) na ni Sehemu ya Safu ya Miliam ya Tao la Mashariki.
No comments:
Post a Comment